Rais Samia Atangaza Maombolezo ya Kitaifa Tanzania Kufuatia Kifo cha Rais Mstaafu Mwai Kibaki

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Taifa jirani la Tanzania linaadhimisha siku mbili za maombolezo kufuatia kifo cha Rais Mstaafu wa Kenya Mwai Kibaki
Rais Samia Suluhu Hassan ametangaza kuwa taifa hilo litamuomboleza Kibaki kwa siku mbili na kuwataka Watanzania kusimama na Wakenya
Kenya nayo ilitangaza Aprili 29 kuwa likizo ya kitaifa kutoa nafasi kwa Wakenya kumuomboleza rais wao wa tatu aliyefariki akiwa na umri wa miaka 90
Tanzania inaadhimisha siku mbili za maombolezo kufuatia kifo cha Rais Mstaafu wa Kenya Mwai Kibaki kilichotokea Ijumaa, Aprili 22, akiwa na umri wa miaka 90.

Rais Samia Atangaza Maombolezo ya Kitaifa Tanzania Kufuatia Kifo cha Rais Mstaafu Mwai Kibaki
Rais Samia Suluhu Hassan ametangaza siku mbili za maombolezo nchini Tanzania kufuatia kifo cha Mwi Kibaki.
Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan ametoa tangazo hilo na kutuma risala za rambirambi kwa taifa la Kenya kwa kumpoteza kiongozi.

Kupitia kwa taarifa iliyotiwa saini na Mkurugenzi wa Mawasiliano katika Ikulu ya Rais Yunus Zuhura, Rais Samia amesema kuwa nchi hiyo itamuomboleza Kibaki kuanzia Ijumaa, Aprili 29 hadi Jumamosi, Aprili 30.

“Rais Samia ametuma risala zake za rambirambi kwa wananchi wa Kenya na kuwahimiza Watanzania kusimama na majirani wao katika wakati huu mgumu wanapomuomboleza aliyekuwa kiongozi wao,” taarifa hiyo inasema.

Bendera itapeperushwa nusu mlingoti nchini kote Tanzania na katika balozi za Tanzania katika mataifa yote ulimwenguni ili kuadhimisha siku hizo za maombolezo ya kitaifa.

Serikali ya Kenya nayo ilitangaza Ijumaa, Aprili 29, kuwa likizo ya kitaifa kumuomboleza Rais Mstaafu Mwai Kibaki, misa yake ya kitaifa ya wafu ikiandaliwa siku iyo hiyo katika uwanja wa kitaifa wa Nyayo.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad