Ahmed Ally Aipiga Kijembe Young Africans "Mmesahau Mzigo Wenu Uwanja wa Taifa"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Meneja wa Habari na Mawasilino wa Klabu ya Simba Ahmed Ally ameipiga kijembe Young Africans kwa kuitaka kuondoa kitu kilichofukiwa katikati ya la Uwanja wa Benjamin Mkapa kabla ya mchezo wa jana Jumatatu (Mei 09) dhidi ya Tanzania Prisons.


Kumekua na mkanganyiko wa nani alifukia kitu hicho katikati ya eneo la kuchezea, kufuatia picha zinazosambaa katika mitandao ya kijamii kuonyesha wachezaji wa Tanzania Prisons wakifanya dua ya pamoja, lakini baadae beki wa kulia wa Young Africans Djuma Shaban alikwenda eneo hilo na kuonekana akifanya jambo fulani.


Ahmed Ally amewaomba Young Africans kukiondoa kitu hicho ili kutoa nafasi kwa timu yao kucheza kwa amani kesho Jumatano (Mei 11) katika mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Kagera Sugar.


Cedric Kaze: Hatufurahishwi na hali hii

“Tunaomba sana Wananchi, kile kutu mlichochimbia jana pale Benjamin Mkapa katikati ya Uwanja, tunaomba mkakifukuwe, kesho tuna mchezo dhidi ya Kagera Sugar, kisije kikatuvunja miguu bure,”


“Halafu, hivi na Prisons nao ni wa kuwaroga kweli, mliroga ili mpate sare? maana yake ni kwamba ndio tabia yenu yaani, isikute hapa ninasema timu ngingi dhaifu, kumbe nyinyi mnawaroga watoto wa watu jamani.”


“Kwa hiyo sasa mkipata ubingwa kwa mfano, mtamsifu Kocha ama Mganga? Msiache kwenda kukifukuwa. Hivi unawezaje kuchimbua uwanja mzuri kama ule wa Benjamin Mkapa? halafu mmetwisha mikoba kijana wa watu wa Congo yule, aaaaaah Wachawi United!” amesema Ahmed Ally


Katika mchezo huo Young Africans ililazimishwa sare ya bila kufungna dhidi ya Tanzania Prisons, huku Mshambuliaji wao hatari kutoka DR Congo Fiston Kalala Mayele akikosa mkwaju wa Penati iliyotokana na Kiungo Feisal Salum kuangushwa eneo la hatari.


Sare hiyo inaifanya Young Africans kufikisha alama 57 ambazo zinaendelea kuiweka kileleni klabu hiyo ya Jangwani, huku Tanzania Prisons ikifikisha alama 23 zinazoiweka kwenye nafasi ya 14.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad