Breaking News: Anayedaiwa Kumuua Mkewe Kwa Risasi Naye Ajiua Kwa Risasi Ziwani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mwanza. Said Oswayo anayedaiwa kumuua kwa kumpiga risasi kadhaa mke wake Swalha Salum (28) naye amekutwa amejiua kwa kujipiga risasi.

Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Mairi Makori amethibitisha kujiua kwa mtuhumiwa huyo ambaye mwili wake umekutwa ndani ya maji ya Ziwa Victoria kwenye ufukwe wa Rock Beach jijini Mwanza.

"Mwili huo umeopolewa ziwani eneo la ufukwe wa Rock Beach ukiwa na majeraha ya risasi kichwani. Timejiridhisha kuwa ndiye mtuhumiwa baada ya kutambuliwa na ndugu zake," amesema Kaimu Kamanda huyo.

Amesema mwili huo ulikutwa unaelea ufukweni mwa Ziwa Victoria ufukwe wa Rock Beach ambapo Jeshi la Polisi lililazimika kuwatafuta ndugu kwa utambulisho na kuthibitisha kuwa mtuhumiwa aliyekuwa anasakwa kwa mauaji ya mke wake.

Taarifa za uhakika zilizopatikana zinaeleza kuwa askari polisi wanaopeleleza tukio hilo walipiga kambi eneo la ufukwe wa Malaika kutokana na mawimbi ya mwisho ya mawaskliano ya mtuhumiwa Oswayo kuonekana eneo hilo kwa mara ya mwisho usiku wa kuamkia jana Mei 29.

"Mawasiliano ya mwisho ya simu ya Oswayo yalifanyika usiku wa manane eneo la Malaika; ndio maana Askari Polisi waliweka kambi pale na kweli mwili wake umepatikana hapo hapo," amesema mmoja wa watoa taarifa wetu kwa sharti la kuhifadhiwa jina
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad