Dkt Abbas Ataja Manufaa Ziara ya Rais Marekani

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo na Mwenyekiti wa Kamati ya Rais ya Kuitangaza Tanzania, Dkt Hassan Abbas amesema kuwa wawekezaji wakubwa zaidi ya watano wameahidi kuja Tanzania baada ya kukutana na Rais Samia nchini Marekani.


Dkt Abbasi ametoa kauli hiyo leo katika mjadala uliokuwa unaendeshwa mtandaoni (Zoom) kuhusu filamu ya Royal Tour


Ametaja baadhi yao kuwa ni mwanadamu anayemiliki hoteli nyingi zaidi duniani, mwingine ni mwanadamu anayemiliki meli nyingi za kifahari kuliko wote Duniani, lakini pia mtu anayemiliki majumba mengi zaidi ya kuonyesha filamu duniani, na alikutana na mwanadamu ambaye anaongoza Kampuni kubwa zaidi ya utalii duniani


Aidha amesema Rais Samia alikutana na mtu anayeongoza mtandao mkubwa kuliko yote duniani ya mawakala wa utalii pamoja na alikutana na watu ambao wanaongoza baraza kubwa zaidi la utalii duniani

Dkt Abbasi amesema watu wote hao wapo tayari kufika Tanzania na taratibu zikikamilika watafika nchini kwa ajili ya shughuli za utalii

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad