Dr Mengi Alitupatia Jengo Sasa Hatulipi KODI - Chama cha Wafanya biashara wanawake Tanzania TWCC

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Chama cha Wafanya biashara wanawake Tanzania TWCC kimesema kimewakuza wafanyabiashara wengi sana wanawake kutokana na mchango wa aliyekuwa mwenyekiti wa makampuni ya IPP Dr Reginald Mengi ikiwemo kuwapatia jengo ambalo hadi sasa ndipo makao makuu ya Chama hicho.



Ni miaka mitatu sasa TWCC kupitia Kwa Mkurugenzi Mtendaji wake Mwajuma Hamza wanamwelezea Dr Mengi kama mtu wa mfano wa kuigwa (mentor) aliyetamani kuwaona watanzania hususani wafanyabiashara wanawake wakikua kibiashara.


"Hili jengo Dr Mengi ametupatia Hadi Leo tunafanya kazi hapa na endapo tungekuwa tumepanga gharama zingekuwa juu sana na kupitia hapa wanawake wengi mno wamenufaika. "alisema Mwajuma hamza Mkurugenzi Mtendaji TWCC.


Pamoja na hayo pia wanamzunguza kama mtu aliyewapa kibali wafanyabiashara wanaweza kupitia vyombo vyake vya habari hali iliyowapa kujulikana zaidi kibiashara hivyo kutoka wito Kwa wafanyabiashara kuyaenzi aliyoyasisi.


"Mwenyekiti aliamini katika kuweza,kufikia malengo na kuwajali watu wenye makundi maalumu wakiwemo wahitaji pamoja watu wenye ulemavu."alisema Mwajuma.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad