Hospitali Yakanusha Madai ya Maiti ya Msanii Osinachi Kuimba Ekwueme usiku

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Hospitali ya Kitaifa ya Abuja, siku ya Jumatatu, Mei 16, ilikanusha madai kuwa maiti ya mwimbaji maarufu wa nyimbo za injili, Osinachi Nwachukwu, ilikuwa ikiimba ‘Ekwueme’ katika chumba cha kuhifadhi maiti.

Hospitali Yakanusha Madai ya Maiti ya Mwimbaji Osinachi Nwachukwu Kuimba Ekwueme Usiku
Hospitali yakanusha madai kuwa maiti ya mwimbaji Osinachi Nwachukwu ilimba Ekwueme usiku. Picha: The Urim & The Thummim.
Msemaji wa hospitali hiyo, Dkt Taiwo Haastrup, alisema hakuna uthibitisho kwamba mwili wa Osinachi ulikuwa ukiimba katika chumba cha kuhifadhi maiti, The Punch inaripoti.

Akiongea na wanahabari, Haastrup alibainisha kuwa mtu aliyekufa hawezi kuimba akiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti.

Osinachi, mwanakwaya katika Kanisa la Kimataifa la Dunamis, alifariki miezi michache iliyopita kutokana na kile kinasemekana kuwa unyanyasaji wa nyumbani aliofanyiwa na mumewe, Peter Nwachukwu.

Sudi Aikashifu Runinga ya Citizen Kwa Kupeperusha Matamshi ya Kiholela ya Junet
Kufuatia kifo chake, mwili wake ulihifadhiwa katika chumba cha maiti cha Hospitali ya Taifa.

Ripoti zilienea kwamba wahudumu wa chumba cha kuhifadhia maiti walidai kuwa maiti ya Osinachi ilikuwa ikiimba wimbo wake wa 'Ekwueme', usiku wa manane.

Akijibu ripoti hiyo, Haastrup alisema: “Kitiba, hakuna kitu kama hicho; ni mawazo ya watu tu. Mtu ambaye amekufa na ni maiti, mtu kama huyo atakuwa anaimbaje usiku?"

"Hakuna chelezo ya matibabu kwa hilo; ni mawazo ambayo yanaweza kuwa ni kutokana na kanisa alilohudhuria akiwa hai, na nyimbo zinaweza tu kuwapa watu mawazo, lakini hakuna uthibitisho kwa njia yoyote. Haiwezi tu kuthibitishwa kwa njia yoyote. “Mtu aliyekufa amekufa na amekuwa maiti; iko ndani ya chumba cha kuhifadhia maiti, haiwezi kuimba na haiwezi kusonga kwa hivyo ni mawazo ya watu."

Kuhusu ripoti ya uchunguzi wa maiti, Hasstrup alisema:

"Ni kesi ya uchunguzi, na ni siri; hatuwezi kufichua chochote hapo. IPO anayehusika atampa IGP, ambaye atapeleka mahakamani. Matokeo yamewasilishwa sawa, na watu wetu walifanya hivyo kwa siri."

Martha Karua: Mgombea Mwenza wa Raila Odinga Akaribishwa Kama Malkia Kirinyaga
Awali, TUKO.co.ke iliripoti kuwa polisi waliwasilisha ripoti ya uchunguzi wa maiti ya marehemu Osinachi.

Hospitali ya Kitaifa, Abuja, ambayo ilifanya uchunguzi wa maiti, ilituma matokeo hayo kwa polisi.

Msemaji wa Federal Capital Territory (FCT) Josephine Adeh pia alikiri kupokea ripoti hiyo katika taarifa yake.


Kuwa wa kwanza kutoa maoni




-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad