Kumekucha...Magari 14 Likiwamo la Ofisi ya RC yakamatwa Songwe

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



KAMATI ya ulinzi na Usalama Mkoani Songwe imekamata magari 14 likiwemo la ofisi ya Mkuu wa Mkoa huo yakisafirisha bidhaa za magendo.

Gari ya ofisi ya Mkuu wa Mkoa iliripotiwa kupotea kwa miaka kadhaa na jitihada za kulifatuta zilikuwa zikiendelea bila mafanikio.

Mkuu wa mkoa wa Songwe Omary Mgumba amesema kuwa dereva wa gari hilo alidanganya kuwa ana dharura na aliondoka na gari hilo, hata hivyo alitoweka na bado anaendelea kutafutwa.

“Tutaendelea kuwashikilia na kuwakamata wamiliki wote wa magari hayo na hawatayatoa hadi pale watakapowaleta madereva wote waliokua wanaendesha magari hayo,” amesema Mgumba.


Aidha Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Mapato Mkoa wa Songwe ametoa wito kwa Wafanyabiashara, kufuata sheria za forodha ili kuepuka kukamatwa na magendo na sheria kuchukua mkondo wake

Habarileo
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad