Miaka 3 Jela Kwa Kuwanyanyasa Kingono yatima Kwenye Kituo chake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Mahakama nchini Misri imemhukumu tajiri mmoja na mfanyabiashara mkubwa aliyekuwa na uhusiano wa karibu na serikali kifungo cha miaka mitatu jela kwa kuhusika katika biashara haramu ya kusafirisha binadamu na shambulio la aibu kwa wasichana wenye umri mdogo katika kituo cha watoto yatima alichoanzisha.


Mohamed El-Amin – ambaye alikuwa anamiliki vyombo vingi vya habari vyenye ushawishi mkubwa, alikamatwa mapema mwaka huu baada ya madai ya unyanyasaji wa kingono katika kituo hicho cha watoto yatima kuwekwa hadharani na shirika la misaada ya kibinadamu liitwalo Missing Children.


Halmashauri zaonywa kutoa mikopo kwa vikundi hewa

Mwendesha mashtaka wa serikali amesema kuwa alitumia mamlaka yake na mazingira magumu ya wasichana hao.


Mamlaka ilifunga kituo hicho cha watoto yatima mwishoni mwa mwaka jana baada ya madai dhidi ya el-Amin kuibuka.


Alikamatwa Januari na tangu wakati huo amekuwa gerezani, El-Amin anaweza kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad