Mkasa wa ndege: Ndege ya China iliyoanguka na kuua watu 132 iliangushwa makusudi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Wafanyakazi wa dharura katika eneo la ajali ya ndege ya China Eastern Airlines
Data za ndege zinaonyesha kuwa ndege ya shirika la ndege la China Eastern Airlines iliyoanguka mwezi Machi iliangushwa kwa kichwa  kimakusudi, kulingana na ripoti za vyombo vya habari vya Marekani.

Wachunguzi hadi sasa hawajapata hitilafu zozote za kiufundi au za kimitambo kwenye ndege hiyo, ripoti zinasema, zikinukuu tathmini ya awali ya maafisa wa Marekani.

Ndege hiyo aina ya Boeing 737-800 ilikuwa ikiruka kati ya miji ya kusini mwa China ya Kunming na Guangzhou ilipoanguka.

Abiria wote 132 na wafanyakazi waliokuwa ndani ya ndege hiyo walifariki katika ajali hiyo.

"Ndege ilifanya kile ilichoambiwa kufanya na mtu kwenye chumba cha marubani," kwa mujibu wa Wall Street Journal, ambalo liliripoti habari hiyo kwa mara ya kwanza, likimnukuu mtu anayefahamu tathmini ya awali ya maafisa wa Marekani kuhusu chanzo cha ajali hiyo.

Data kutoka kwa kifaa kimoja cha kurekodia ndege cha "black box" ambacho kilipatikana kutoka eneo la ajali, ilipendekeza kwamba maagizo kwenye vidhibiti viliisukuma ndege hiyo wima kwenda chini, ripoti hiyo ilisema.

Habari za ABC, zikiwanukuu maafisa wa Marekani, pia ziliripoti kwamba ajali hiyo inaaminika ilisababishwa na kitendo cha kukusudia.

Wachunguzi wanaochunguza ajali hiyo wanachunguza iwapo ilitokana na hatua za kimakusudi kwenye staha ya ndege, bila ushahidi uliopatikana wa hitilafu ya kiufundi, kulingana na Reuters, ambayo ilitaja watu wawili waliofahamishwa kuhusu suala hilo.

Shirika la ndege la China Eastern Airlines hapo awali lilisema marubani watatu waliokuwa kwenye ndege hiyo walikuwa na sifa na afya njema.

Shirika la ndege kando liliambia Wall Street Journal kwamba hakuna dalili kwamba yeyote kati ya marubani alikuwa katika matatizo ya kifedha.

China Eastern Airlines haikujibu mara moja ombi la BBC la kutoa maoni.

Utawala wa Usafiri wa Anga wa China (CAAC), ambao unaongoza uchunguzi katika ajali hiyo, pia haukujibu mara moja ombi la BBC la kutoa maoni.


Mwezi uliopita, CAAC ilisema ripoti kwamba huenda ndege hiyo ilianguka kimakusudi "zimepotosha sana umma" na "kuingilia kazi ya uchunguzi wa ajali".

Wachunguzi bado wako katika mchakato wa kuchambua data ya ndege na mabaki ya ajali hiyo, chombo cha habari cha serikali ya China kiliripoti Global Times Jumatano. 

Pia ilisema CAAC itaendelea "kufanya uchunguzi wa ajali kwa njia ya kisayansi na utaratibu". 

Ubalozi wa China mjini Washington, Bodi ya Kitaifa ya Usalama wa Usafiri wa Marekani (NTSB), na watengenezaji ndege wa Boeing walikataa kutoa maoni yao kuhusu ripoti ya Wall Street Journal, kutokana na miongozo iliyowekwa na Shirika la Kimataifa la Usafiri wa Anga la Umoja wa Mataifa.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad