Mtoto wa Mbunge Ajipiga Risasi na Kujiua Nyumbani Kwao

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mwanawe wa Kiume wa Mbunge Sankok Kutoka Kenya Ajipiga Risasi na Kujiua Nyumbani Kwao

Memusi Sankok, mwenye umri wa miaka 15, inadaiwa alijifyatulia risasi kwa kutumia bastola ya baba yake mzazi siku ya Jumatatu, majira ya mchana.

Inasemekana aliichukua bastola hiyo, iliyokuwa imefichwa kwenye sanduku salama, kwenye bafu ya baba yake.

Mwanawe wa kiume wa Sankok alikuwa mwananfunzi wa kidato cha nne, katika Shule ya Upili ya Kericho.


Haijabainika ni kwa nini Memusi aliamua kuchukua hatua hiyo ya kujitoa uhai, huku uchunguzi wa mkasa huo ukiendelea.

Familia ya Mjukuu Feki wa Kibaki Yazungumza, 'Alikuwa tu Anatafuta Kazi'
Bastola hiyo iliyokuwa ikitumika na Mbunge huyo na kusababisha mauai ya mwanawe, tayari imetwaliwa na maofisa wa polisi wa Idara ya Ujasusi wa Jinai (DCI) ili ikaguliwe.

Akithibitisha kisa hicho, Naibu Kamishna wa kaunti ndogo ya Narok Kusini (DCC), Felix Kisalu alisema maofisa wa DCI wameanzisha uchunguzi kuhusiana na tukio hilo.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad