Mtoto wa Rais Museven afikishwa mahakamani kwa kuutaka Urais wa baba yake

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mahakama ya kikatiba ya Uganda imemtaka mtoto wa Rais Yoweri Museveni, Luteni Jenerali Muhoozi Kainerugaba, kujibu shtaka analotuhumiwa la kueleza nia yake ya kuwania urais akiwa bado anahudumu katika jeshi la nchi hiyo, tovuti ya Daily Monitor imeripoti.

Wakili wa haki za binadamu Gawaya Tegulle aliiomba mahakama katika mji mkuu, Kampala, kumzuia Jenerali Kainerugaba kufanya shughuli za kisiasa akiwa bado anatumikia jeshi.

Gawaya pia anataka jenerali huyo afunguliwe mashtaka ya uhaini kufuatia madai yake ya njama ya kumrithi babake kwa kutumia mbinu "haramu".

Jenerali Kainerugaba, kamanda wa jeshi la nchi kavu la Uganda, ana siku 10 kuwasilisha majibu yake. Mnamo tarehe 2 Mei, alitangaza mipango ya kuzindua mpango wa kisiasa, na kuchochea uvumi kwamba alinuia kumrithi babake wa muda mrefu.


 
Mnamo Machi 8, alitangaza kustaafu kutoka kwa jeshi kwenye Twitter lakini Rais Museveni alikataa. Rais Museveni amekanusha kumuandaa mwanawe kuchukua wadhifa wake.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad