Ugonjwa wa Monkey Pox Wahatarisha Ulimwengu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Shirika la Afya ulimwenguni (WHO), limethibitsha ripoti ya nchi 12 zilizoonesha matukio 80 ya

uwepo wa ugonjwa wa Monkeypox na kwamba bado wanachunguza madai mengine 50 ya

maradhi hayo na kuonya Mataifa Ulimwenguni kuchukua tahadhari.


Kwa mujibu wa Taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa WHO kanda ya Ulaya Dkt. Hans Henri Kluge

imetaja nchi hizo kuwa ni Ujerumani, Sweden, Ubelgiji, Ufaransa, Italia, Ureno, Uhispania na

Uingereza.


“Maambukizi ya ugonjwa huo unaoharibu ngozi pia yamethibitishwa katika nchi za Ulaya,

Amerika, Canada na Australia lakini kwa Afrika unapatikana katika sehemu za mbali za Afrika ya

Kati na Magharibi,” ameongeza Kluge.


Ugonjwa huo ambao unasababisha na virusi kutoka kwa Wanyama kwenda kwa binadamu barani Afrika unatajwa kutokea katika jamii zilizopo karibu na misitu ya Afrika ya kati na Magharibi kuliko na hifadhi za Wanyama.


Dkt. Kluge amesema matukio ya wagonjwa wa Monkeypox yamegunduliwa katika kliniki

maalumu za magonjwa ya zinaa na kwamba maambukizi hayahusishi muingiliano wa safari

ingawa mapenzi ya jinsia moja kwa wanaume ni moja ya sababu.


“Hata hivyo dalili za wagonjwa waliogundulika barani ulaya zinaonesha kufanana na zile

zilizoripotiwa siku za karibuni katika nchi za Australia, Canada na Marekani ila hakuna uhusiano wa kimaambukizi kulingana na muingiliano wa wasafiri,” amefafanua Kluge.



Mtoto mwenye Monkeypox

Aidha Dkt. Kluge amebainisha kuwa WHO inaendelea kufanya uchunguzi kwa nchi ambazo

ugonjwa huo umeibuka ili kupata taarifa zitakazosaidia ugunduzi wa matukio mengine ingawa mpaka sasa haijulikani kiwango cha maambukizi kilichopo kwenye jamii.


“Kwa sasa dalili ni ndogo na wengi wa walio ambukizwa watapona ndani ya wiki chache bila

matibabu ila ugonjwa huu unaweza kuwa mkali zaidi hasa kwa watoto wadogo, wanawake

wajawazito na watu ambao hawana kinga mwilini.” ameelekeza DKt. Kluge.


Ugonjwa wa Monkeypox huambukizwa kwa kugusana na mtu mwenye vidonda kwenye ngozi,

kuvuta hewa yenye matone ya mtu aliye na ugonjwa huo au maji maji ya mwilini, kujamiiana, au kuchangia vitu na mtu aliyeambukizwa.


WHO inaelekeza kuwa dalili za ugonjwa huo zinaweza kuwa ndogo lakini vipele vinavyotokea

kwenye ngozi huwasha na kuleta maumivu na imetoa wito kwa yeyote aliye na dalili za vipele

visivyo vya kawaida kuwahi hospitali ili kupata ushauri wa watoa huduma za afya.


Bado hakuna tiba maaalum ya Monkeypox lakini chanjo ya ugonjwa wa ndui inatajwa kutoa kinga kwa asilimia 85 kwa kuwa virusi hivi viwili ni familia moja na uwezekano wa kuambukizwa ni mdogo.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad