"Anajua Ukichaa Wangu Wote" Harmonize Aahidi Kumnunulia House Girl Wake Gari na Nyumba

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Staa wa Bongo Rajab Abdul Kahali almaarufu Harmonize ameahidi kumzawadi mjakazi wake Zuwena kwa nyumba na gari.

Amepiga hatua hiyo kama ishara ya shukran kwa huduma alizomtolea katika kipindi cha miaka saba ambacho kimepita.

Konde Boy ametangaza kuwa anapanga kutimiza hadi yake kwa Zuwena kabla ya mwezi wa Mei kuisha.


"Ni kama shangazi yangu. Miaka 7 anajua nakula nini. Ananipikia, ananifulia, ananifanyia usafi, anajua ukichaa wangu wote. Kabla ya Juni namnunulia gari lake la kwanza na kinyumba hata cha chumba 3 mkoani kwao," Harmonize alitangaza kupitia Instagram.

Harmonize amefichua kuwa Zuwena ndiye mjakazi wake wa kwanza huku akidai kuwa sio kijakazi wake tu bali pia ni kama dada yake.

Amemshukuru sana mwanadada huyo kwa kazi kubwa ambayo amekuwa akifanya na kumtakia baraka za Maulana.

"Mungu akubariki dada Zuuh maana si kwa vipipi vya sigara ambavyo unavifagia kila siku kwenye mashuka majivu vipi," Aliandika.


Mwanamuziki huyo aliambatanisha ujumbe wake kwa video ya Zuwena akiwa jikoni akipakua chakula.

View this post on Instagram
A post shared by Zuwena Salum (@chef_zuwena)

Siku za hivi majuzi Harmonize amekuwa akiwanunulia watu wa karibu naye magari kwa sababu tofauti.

Tayari amemnunulia magari mawili aliyekuwa mpenzi wake Kajala Masanja akiwa na nia ya kuomba msamaha na kurejesha mahusiano ya.


Mapema wiki hii alimnunulia mama yake mzazi gari aina ya Harrier na kufichua kuwa hiyo ndiyo gari aipendayo zaidi.

Mwezi uliopita alimnunulia gari ndogo mpiga picha wake Jabulant.


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad