Ali Kambwe 'Mambo 10 nilioyaona Mabingwa Yanga vs Coastal Union, Kuna Mabingwa wa Michongo na Kuna Mabingwa wa Mpira"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Mambo 10 nilioyaona Mabingwa Yanga vs Coastal Union


1: YANGA BINGWA🏆 PESA YA GSM, AKILI YA HERSI SAID, BUSARA YA MSOLLA NA UMOJA/UPENDO WA MASHABIKI UMEIFANYA TANZANIA KUWA YA NJANO NA KIJANI 💛💚


2: UNBEATEN CHAMPION ✊ YANGA BINGWA BILA KUPOTEZA MCHEZO. YANGA BINGWA AKIWA NA MECHI 3 MKONONI👏 QUALITY. QUALITY. QUALITY! Hivi ndio hadithi Fupi ya Yanga kwa msimu wa 2021/2022


3: BILA SHAKA JUMA MGUNDA AMEPATA DAKIKA 90 zenye somo kubwa kwake kuelekea Arusha kwenye Fainali.. Somo kubwa la mbinu! Ni kujiweka kitanzi shingoni kucheza na Yanga na ukawapa Faida ya namba Katikati ya uwanja. Kivipi?


4: Coastal Union walikuwa na mfumo wa 4-4-2 na walibadilika kwenye 4-2-4 wakishambulia. Mstari wao wa kwanza wa ulinzi wakachagua uwe wa juu [High Line Pressing]. Yanga wakawa na Quality ya kudili na presha yao Lakini Coastal wakamkosa kiungo mzuri wa chini wa kudili na ubora wa Feisal Salum


5: Yanga kwenye 4-3-3 .. Dickson Job na Bangala ni wazuri kwenye ‘Build Up’ .. Aucho na Sure Boy ni wazuri kwenye pasi.. Sopu alipokuwa na akili ya kushambulia tu, akaicha safu yake ya kiungo ikiwa kwenye muundo wa 2v3. Hii ikawa hatari sana kwao kucheza kwenye High Line


6: MAYELE✊ Top Striker! Mabao yake 16 msimu huu ukiyaweka kwenye tathimini nzuri utabaini idadi ya pointi alizochangia kwenye kuamua mechi.


7: NAMKUBALI SANA YANICK BANGALA! Ni vile tu tuko kwenye dunia inayoabudu namba kwenye mpira Lakini kwangu NI BANGALA ANASTAHILI KUWA MCHEZAJI BORA WA YANGA MSIMU HUU. Uwezo wake wa kubadilika uwanjani, utulivu kwenye maamuzi.. What A Player✊


8: Asante Nabi👏 Moja katika sajili bora alizofanya katikati ya msimu ni SURE BOY! Sure alikuja na Plan B ya Ufundi uwanjani.. Yanga waliweza kuwa na Approach tofauti wakiwa na Sure boy! What A Signing 🙌


9: Yule Akpan anajua mpira! Vicent Aboubakar asante kwa jasho lako! Wenye macho wameona. Fighting Spirit yake kwenye kugombania mpira wa pili kati yake na Farid Mussa ulikuwa kivutio sana uwanjani


10: DJUMA SHABANI 👏 ile Movement ya FeiToto.. Ile pasi yake kwa Mayele ni Class ya viwango vya juu sana! Well Done WANANCHI! Mmejua kumwagilia mioyo ya mashabiki wenu


Nb: Kuna Mabingwa wa michango na KUNA MABINGWA WA MPIRA 😃

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad