Gigy Money Adai Unga, Pombe Vinatesa Mastaa wa Bongo, Agusia na Bangi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Gigy Money mwanadada anayetamba na kibao cha Pressure alichomshirikisha Whozu

GIFT Stanford almaarufu Gigy Money; ni mwanamama staa wa muziki nchini Tanzania ambaye amefichua siri ya mastaa wengi Bongo kuwa wana njaa inayowasababisha kuishia kuteswa na matumizi ya madawa ya kulevya (unga), bangi na pombe.

 

Gigy anasema kuwa kibaya zaidi hawana elimu ya matibabu ya kuondokana na msongo wa mawazo na kuishia kulalamika wasijue namna ya kujinasua huko.

 

“Mastaa wengi wa Bongo wanaishi kwenye njaa mpaka unawakuta wamepigwa picha wakiwa wamekondeana kwa sababu ya cocaine (unga), weed (bangi) na alcohol (pombe).


Gigy Money na Whozu

“Na kibaya zaidi Wabongo wengi hawajui kufanya therapy (tiba ya kuathirika na msongo wa mawazo) na ninamshukuru sana marehemu Ruge Mutahaba ndiye aliniambia ninahitaji mtu wa kuniweka vizuri kisaikolojia, therapist; mtu wa matibabu ya akili ni mambo ambayo wanapaswa kujifunza,” anasema Gigy ambaye ni mama wa mtoto mmoja.

Cc; @sifaelpaul

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad