Kutana na Mwanamke Anayeogoa Mara NNE Kwa Siku Kisa Ana Ugonjwa wa Kunuka Kama Samaki

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Kwa huzuni mwanadada Kelly(41) kutoka nchini Uingereza amesema kila siku inamlazimu kuoga sio chini ya mara nne kwasababu amezaliwa na tatizo la kutoa harufu mbaya kama samaki aliyeoza na hali hiyo hujionesha hadi katika mkojo


Kelly amesema alianza kujigundua kuwa ana harufu ya tofauti akiwa na miaka 6 tu lakini hakujua hasa tatizo hilo linatokana na nini hadi alipofikisha miaka 34 ndio akaelewa vizuri


Amesema inamlazimu kuoga mara nne kwa siku na kujipulizia pafyumu/deodorant kila wakati lakini ndani ya muda mfupi tu tatizo linarudi tena. Amesema ametumia sabuni za kila aina kuogea lakini wapi sana sana mwili ukiwa katika uasili wake kidogo kuna afadhali


Ameongeza kuwa baadhi ya watu wasiojua tatizo hilo humsema vibaya wakidhani sio msafi mara unene ndio chanzo apungue lakini anasema ukweli ni tofauti kwani alipokuwa mwembamba hali ilikuwa hivyo hivyo na pia yeye ameajiriwa sekta ya afya(radiographer) hivyo watu kudhani labda ni mchafu inamfanya ajisikie vibaya hadi kulazimika kwenda kwa wanasaikolojia na hata kazini anapendelea zaidi zamu za usiku


Amesema akikaa karibu na watu anaonekana kama kero flani hivi. Pia kuna baadhi ya vyakula kama maini, figo, maharage, karanga etc hatakiwi kula kwani vinachochea ukubwa wa tatizo hilo na Kuna vyakula ameshauriwa ale kupunguza ukali wa tatizo


Katika lugha rahisi tatizo hilo linajulikana kama Fish-Odour Syndrome na hadi sasa rekodi za dunia zinaonesha watu 100 tu ndio wana tatizo hilo lakini wataalam wanasema kuna uwezekano wapo watu wengine kukaribia hata 200 ambao rekodi zao bado kukusanya


Watu wenye tatizo hilo wengine hutoa harufu Kama ya samaki waliooza, kinyesi etc. Na inaelezwa wataalam bado hawajagundua dawa ya kuondoa au kuponesha tatizo hilo moja kwa moja


Kelly amesema ameamua kuzungumza kuhusu hali yake ilimkutoa elimu kwa wasiofahamu hali hiyo

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad