Mauaji Mengine ya Kutisha, Mume Amuua Mchepuko Kisha Yeye Kunywa Sumu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Marehemu Bunanzi Kulwa
KATIKA hali ya kusikitisha Mwanaume mmoja aliyefahamika kwa jina la Bunanzi Kulwa maarufu kama Ngosha Mkazi wa Mbagala kwa mbiku jijini Dar es salaam anadaiwa kumuua mpenzi wake aliyefahamika kwa jina la Happines Zakarika kisha nae kujiua kwa kunywa sumu, huku chanzo kikiwa bado hakijajulikana

Tukio liho limetokea Juni 8 mwaka huu, huku likizua sintofahamu kwa majirani wa eneo hilo kutokana na marehemu hao kuishi kama dada na kaka kwa takribani miaka 2.

Waandishi wetu Issa mnaly na Richard Bukos wamefika eneo la tukio na kuzungumza kwa kina na Rafiki wa karibu wa Marehemu Ngosha aliyejitambulisha kwa jina la Shineneko Ruge ambaye anabainisha kuwa marehemu alikuwa ni rafiki yake wa karibu.


Shineneko Ruge rafiki wa Marehemu
Ruge amesema kuwa usiku mmoja kabla ya kifo cha marehemu alimpigia simu mama yake mzazi na kumuambia kuwa atajitoa uhai.


 
Aidha Ruge amebainisha kuwa siku moja kabla ya kufariki alikuwa na rafiki yake huyo ambaye kwa sasa ni marehemu na moja kati ya maongezi yao ni kwamba alimuaga kuwa atasafiri yeye na dada yake kwenda Marekani hivyo alikuwa akifuatilia masuala ya Visa, lakini Ruge anasikitika kwa kusema kuwa hakufahamu kama hiyo ndiyo ilikuwa safari yake ya mwisho hapa duniani.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad