Mawakili wa Mfalme Zumaridi waomba ahamishwe

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mawakili wa upande wa utetezi katika inayomkabili Mfalme Zumaridi na wenzake wameiomba Mahakama ya Hakimu Mkazi Mwanza kama itawezekana mteja wao awekewe ulinzi au ahamishwe katika Gereza Kuu la Butimba alililopo hivi sasa kufuatia kuwepo kwa taarifa za kuuawa kwake ndani ya gereza.


Ombi hilo la Mawakili wa upande limewasilishwa hii leo Juni 17, 2022, ambapo Hakimu Mkazi wa Mahakama hiyo Monica Ndyekobora, akawataka Mawakili hao kufikisha malalamiko hayo kwa uongozi wa Gereza Kuu la Butimba kwa ajili ya hatua zaidi huku akiahirisha kesi hiyo hadi tarehe 30 ya mwezi huu.


Mfalme Zumaridi pamoja na wenzake wanakabiliwa na kesi ya kufanya mkusanyiko usio halali na imeanza kutolewa ushahidi ambapo leo hii shahidi namba moja ametoa ushahidi mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi mkoa wa Mwanza.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad