Polisi yamsaka Mume Anayedaiwa Kumuua Mkewe

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Dar es Salaam. Jeshi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam linamtafuta mkazi wa Mazizini Ukonga kwa tuhuma za kumuua mke wake, Logesara Chitemo kwa kumchoma na kitu chenye ncha kali.

Kamanda wa Polisi Kanda hiyo, Jumanne Muriro amesema tukio hilo lilitokea Juni 6, 2022 ambapo marehemu alikuwa anauza pombe ya kienyeji ndipo walianza ugomvi ambapo mume wake.

Amesema kuwa baada ya kuibuka ugomvi kati ya wawili hao, mume alimchoma mkewe na kitu chenye ncha kali na kumsababishia majeraha kifuani na kichwani na baadaye kufariki dunia.

Kamanda Muliro amesema mtuhumiwa huyo baada ya kufanya kitendo hicho alikimbia kusikojulikana.


"Jeshi la Polisi linaendelea kumtafuta mtuhumiwa huyo na lazima tutampata na tutamfikisha kwenye vyombo vya sheria,"amesema Muliro.

Ametoa rai kwa wananchi pale inapotokea migogoro kwenye familia kushirikisha ndugu au taasisi za kidini na vyombo vya kisheria kikiwamo ya ustawi wa jamii pamoja na mahakama ili kutatua migogoro hiyo.

Kamanda Muliro amesema oparesheni ya kuzuia vitendo vya uhalifu katika Jiji la Dar es Salaam inaendelea ambapo vikosi mbalimbali vukiwamo vya mbwa na farasi vinafanya doria maeneo ya Cocobeach, Cocomihogo na Coco Plaza.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad