Simon Msuva azianika Simba SC, Young Africans

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Kiungo Mshambuliaji wa Tanzania Simon Msuva, amethibitisha kufuatwa na viongozi wa klabu za Simba SC na Young Africans SC, ili akubali kujiunga nazo kwa ajili ya msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara na Michuano ya Kimataifa.


Msuva ambaye kwa sasa ni mchezaji huru kufuatia kuachana na Mabingwa wa Soka Barani Afrika upande wa vilabu Wydad Casablanca, yupo nchini Tanzania kwa zaidi ya miezi mitatu akifanya mazoezi binafsi ya kujiweka ‘FIT’.


Kiungo huyo ambaye aliwahi kucheza Young Africans kabla ya kutimkia Morocco, amesema kwa nyakati tofauti viongozi wa klabu za Simba SC na Young Africans wamemfuata kumshawishi ili ajiunge nao kwa msimu ujao, lakini hadi sasa hajafanya maamuzi yoyote.


Sogne amaliza ubishi, Aziz Ki atacheza Young Africans

Hata hivyo Msuva amesema huenda akakubali kujiunga na moja ya timu hizo kubwa nchini Tanzania, hivyo amewataka Mashabiki wa soka nchini kuendelea kuwa na subra.


“Timu zote kubwa za hapa nchini zimenifuata kwa ajili ya mazungumzo ya kunisajili lakini bado sijafikia muafaka kwa kuwaomba wanipe muda . Kati ya timu hizo basi mojawapo huenda nikajiunga nayo.” Amesema Msuva


Matola afichua siri ya kuibanjua Mbeya City

Mara ya mwisho Msuva alionekana Dimbani akiwa na kikosi cha Cambiaso Sports wakati wa mchezo wa Kirafiki dhidi ya Simba SC uliopigwa Mo Simba Arena, jijini Dar es salaam.


Katika mchezo huo Msuva aliifungia Cambiaso Sports mabao mawili, huku Simba SC ikiibuka na ushindi wa mabao matatu

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad