Wamaasai Dar Waandamana Kukemea Upotoshaji

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 

Kundi la jamii ya Kimaasai waishio Dar es Salaam, leo Juni 17, 2022, wameandamana katika Ubalozi wa Kenya na kuiomba serikali ya Kenya kuingilia kati upotoshwaji wa zoezi linaloendelea Ngorongoro, unaofanywa na Asasi za Kiraia pamoja na wanaharakati waishio nchini humo.


Wamaasai kutoka maeneo mbalimbali wamefanya maandamano ya amani hadi Ubalozi wa Kenya Tanzania, kuiomba serikali ya Kenya iingilie kati upotoshaji unaofanywa na asasi za kiraia na wanaharakati katika zoezi la kuhama kwa hiari linaloendelea katika wilaya ya Ngorongoro pamoja na tarafa ya Loliondo.


Wamasai hao wameeleza kuwa upotoshaji huo umelenga kuichonganisha jamii ya Wamaasai na serikali ya Tanzania, pamoja na kuzorotesha jitihada mbalimbali za makubaliano zilizofikiwa na pande zote mbili.


hayo yameelezwa kupitia barua ya pamoja iliyosainiwa na Katibu wa Umoja huo anayetambulika kwa jina la Loishiye Lashilunye iliyosomwa na kiongozi wa msafara aliyejitambulisha kwa jina moja la Emanuel.


hatua hii inakuja baada ya zoezi la kuweka alama za mipaka katika eneo la Loliondo pamoja na uhamaji wa wananchi wa Ngorongoro ambapo licha ya serikali kutanabaisha uwepo wa makazi mapya katika eneo la Handeni, kumetokea upotoshaji na uchochezi unaolenga kukwamisha zoezi hilo

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad