Zari Kanunua Nyumba?, Azindua Mjengo wa Kifahari Nchini Kenya

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


ZARI The Boss Lady; ni mwanamama tajiri Afrika Mashariki na Baby mama wa staa wa muziki wa Tanzania, Diamond Platnumz ambaye wikiendi iliyopita alikuwa nchini Kenya akizindua mjengo mpya anaodaiwa kununua jijini Nairobi.


Nyumba hiyo aliyozindua ina mtindo wa ndani wa kipekee ambao hakuna kwa Afrika Mashariki.

Kwa mujibu wa Zari, alikuwa nchini Kenya kwa ajili ya kununua nyumba katika Jiji Kuu la Kenya, Nairobi.

Alisema; “Niko huku kwa uzinduzi wa nyumba ya kifahari iliyojengwa kwa mtindo wa kisasa, ni mojawapo ya majumba usiyotarajia kuyaona Afrika Mashariki.”



Zari Hassan maarufu kama Zari The Boss Lady amefanikiwa kupata watoto wawili akiwa na Staa wa muziki Afrika Diamond Platnumz kutoka Tanzania


Zari mwenye umri wa miaka 42 ni mfanyabishara kutoka nchini Uganda anayeishi nchini Afrika Kusini. Alizaliwa mjini Jinja huko Uganda, wazazi wake ni Waganda kwa kuzaliwa.


Kiwango kikubwa cha utajiri wake kimetokana na uwekezaji katika nyanja za mali isiyohamishika au real estate, hoteli za kifahari za nyota tano huko Kampala na Shule ye Brooklyn huko Afrika Kusini.


Wapo wanaosema amenunua mjengo huo, lakini wengine wanasema alikwenda kufanya uzinduzi tu kwa kuwa ni balozi wa kampuni ya real estate (ya kununua na kuuza nyumba).

Cc; @sifaelpaul


-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad