Auawa Baada ya Kuiba Milioni 19 na Vocha

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Mtu mmoja anayedhaniwa kuwa ni jambazi, ameuawa kwa risasi na jeshi la polisi, baada ya yeye na wenzake watatu kuiba pesa zaidi ya shilingi milioni 19 na vocha za simu za mkononi, kutoka katika duka la mfanyabiashara Musa Maduhu wa kijiji cha Nemba, wilaya ya Biharamulo mkoani Kagera.


Kamanda wa polisi mkoani Kagera William Mwampaghale, amesema kuwa wizi huo ulifanyika Julai 12 mwaka huu, na kwamba baada ya polisi kupata taarifa waliweka mtego na kufanikiwa kuwapata katika Kijiji cha Mgera, Kata Nyantakala wilayani humo, wote wanne wakiwa wamepanda pikipiki moja, na waliposimamishwa wakakaidi,  polisi wakafyatua risasi na kuwajeruhi watu wawili.


"Mtu mmoja ambaye hajafahamika jina alifariki wakati anapelekwa hospitalini, huku wengine watatu akiwamo mmoja aliyejeruhiwa kwa risasi walifanikiwa kutoroka na tunaendelea kuwatafuta, katika eneo la tukio kulipatikana pikipiki iliyotumiwa na wahalifu hao yenye namba za usajili MC 489 DJH, fedha noti za shilingi 355,000 na sarafu shilingi 22,250" amesema RPC Kagera Mwampaghale

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad