AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Duru zinaarifu kuwa Rais ameanza kufunga virago tayari kuenda kuanza maisha yake kama raia baada ya kuwa uongozini kwa miaka 10.
Rais alichukua hatamu za uongozi 2013 alipokabidhiwa upanga na aliyekuwa rais Mwai Kibaki.
Kwa mujibu wa runinga ya KTN, wafanyakazi wa Ikulu wamekuwa wakiondoa mali ya kibinafsi ya Uhuru na familia yake katika maandalizi ya kupungia Ikulu mkono.
Uhuru amekuwa akitangaza kuwa yuko tayari kupeana mamlaka kwa mgombea wa urais atakayeshinda.
Akiongea Ijumaa Julai 8 katika Ikulu, Rais alisema amechoka na changamoto za kuwa rais na anasubiri sana kuenda kupumzika.
"Sitaki kuendelea kuwa mamlakani kama vile wanasema. Hii kazi ni ngumu sana, hakuna kulala . . . nyumba imejaa changamoto na miaka kumi ambayo nimekuwa hapa imetosha. Nasubiri sana Agosti 9," alisema Kenyatta.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK