AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amemwachisha kazi waziri aliyetajwa katika uchunguzi wa ubakaji, katika mabadiliko ya baraza la mawaziri baada ya muungano wake tawala kupoteza wingi wa viti katika uchaguzi wa bunge.
Ikiwa tu ni mwezi mmoja na nusu baada ya mabadiliko yaliyopita, mawaziri wa mambo ya kigeni, fedha na ulinzi walibaki katika nyadhifa zao lakini Macron alifanya mabadiliko katika nyadhifa nyingine muhimu.
Mkurugenzi wa shirika la Msalaba Mwekundu la Ufaransa Jean-Christophe Combe ameteuliwa kuwa waziri mpya wa mshikamano na uwiano wa kijamii baada ya tuhuma dhidi ya Damien Abad, ambaye anakanusha kufanya kosa lolote, katika kashfa ambayo imeiaibisha serikali.
Mchumi mkuu wa Shirika la Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo Laurence Boone ameteuliwa kuwa waziri mpya wa masuala ya Ulaya.
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK