Ajali ya basi: 45 wanusurika kifo

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Watu wasiopungua 45, wamenusurika kifo huku wengine 13 wakipata majeraha wakati basi la kifahari lilipotumbukia kwenye mtaro wa maji katika barabara ya Ejule-Ochadamu iliyopo Halmashauri ya Ofu, Jimbo la Kogi nchini Nigeria.


Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani cha Shirikisho la Sekta ya Jimbo la Kogi (FRSC), Stephen Dawulung amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo na kusema tukio hilo lilitokea majira ya saa nane mchana Septemba 6, 2022.

 

Amesema, majeruhi hao 15 walipelekwa katika Hospitali ya Grimard, Anyigba na Hospitali ya Holy Memorial kwa matibabu huku walionusurika wakiruhusiwa kuendelea na safari.


Kufuatia ajali hiyo, Dawulung amewaonya madereva kuacha tabia ya kuendesha magari kwa mwendo kasi, kwani mara zote huwa ni chanzo cha ajali na vifo kwenye barabara kuu.


Inadaiwa kuwa Dereva wa basi hilo alipoteza mwelekeo kutokana na hitilafu ya breki na chanzo cha kutumbikiza basi mtaroni kilitokana na mwendokasi.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad