Jamaa Ampachika Mama Yake Mimba, Mkewe Amtetea

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Katika miaka ya zamani na leo, watoto huchukuliwa kama zawadi kwa familia, Mama mjamzito hutunzwa kama yai. Mtoto hua mwanga wa furaha kwa wanandoa.

Nchini Marekani, mwanamke mwenye umri wa miaka 56 kutoka eneo la Utah anakila sababu ya kutabasamu wiki chache zijazo atakapo tanabahiwa na mtoto wake na mwanawe wa kumzaa. Hii ni baada ya kugundua mkazamwana hana uwezo wa kushika mimba.

Jeff na mke wake ambao ni wazazi wa watoto wanne walikuwa wamehangaika kupata mimba kwa miaka sita kabla ya kupata mapacha, Vera na Ayva wa miezi 11 kisha Diseal na Luka.


Hata hivyo, mipango yao ya kuwa familia kubwa iligonga mwamba mwaka jana kufuatia upasuaji wa kuzaliwa kwa mapacha hao.

Baada mamake Jeff kujua hali yao, aliingilia kati na kujitolea kuwasaidia baada ya kujua kwamba anaweza kujifungua licha yake kuwa mkongwe.

"Sikuwahi kufikiria hili litafanyika, lakini baada ya mkewe Jeff kujifungua kwa dhiki na kuniomba nimbebe mtoto wao. Niliwaambia niko tayari lakini ningali mzee. Lakini baada ya kushauriana na madaktari walisema mimi ni mzima na nina afya njema," Nancy aliiambia kituo kimoja cha habari huko Marekani.

Sasa baba wa familia hiyo yupo tayari kumpokea mtoto wake wa tano.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad