Mchungaji Aliyehaidi Akifa Atafufuka Mwaka Sasa Umepita Hajafufuka Baada ya Kufariki

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Mchungaji maarufu kutokea Afrika Kusini ambaye alifariki dunia mwezi Agosti 2021, mpaka hii leo bado yupo ndani ya chumba cha kuhifadhia maiti kilichopo katika Jimbo la Gauteng, Johannesburg nchini humo baada ya kushindwa kufufuka kama alivyoahidi.

Siva Moodley ana kundi la Wafuasi ndani na nje ya Afrika Kusini na anaheshimika miongoni mwa jumuiya ya kidini kwasababu ya ‘miujiza’ aliyoifanya wakati wa mahubiri yake pale alipokuwa hai.

Mitandao ya South Africa imeripoti kuwa tangu kifo chake karibia siku 400 zilizopita, Mchungaji Moodley amehifadhiwa kwenye nyumba ya kuhifadhia maiti iitwayo Martins Funeral Home, Taasisi hiyo, iliyoko Fourways, imelipwa ili kumweka Kiongozi huyo wa imani katika uangalizi wao lakini hata mtiririko wa pesa wa karibia R60 000 (Tsh. 8,137,595) uliotolewa kama bima ili kuhifadhi mwili huo unaanza kupungua.

Martin du Toit anayeendesha nyumba hiyo ya kuhifadhia maiti, hivi karibuni alisema anaomba idhini kutoka kwa Mahakama ili kuchoma mwili huo, huku ikionekana kuwa hata Wafusi wake wamekata tamaa juu ya ufufuo wake kwasababu mwili wake haujatembelewa na Mtu yeyote kwa zaidi ya miezi 12 sasa.

Inasemekana kuwa Mzer huyo wa miaka 53, ambae alikuwa Mwanzilishi wa Kaniaa la ‘The Miracle Centre’ lililoko kaskazini mwa jiji la Johannesburg alifariki dunia tarehe 15 Agosti mwaka jana baada ya kuugua, Kanisa lake halijakiri kifo chake kwenye mitandao yao ya kijamii mpaka leo, na akaunti zake za Twitter bado zipo active na kujibu Watu kama vile ni yeye.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad