Mike Sonko Akerwa na Jinsi Marais wa Afrika Walivyorundikwa Kwenye Basi Jijini London

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mike Sonko, hakuficha jinsi alivyokereka na hatua ya Marais wa Afrika, kulazimishwa kuabiri basi moja walipohudhuria mazishi ya Malkia wa Pili wa Uingereza
Kwenye picha iliyozagaa mitandaoni, Rais William Ruto alionekana ameketi sako kwa bako ndani ya basi hilo, na mkewe ambaye ni Mama wa Taifa Racheal Ruto

Picha hiyo imeonekana kumuudhi sana Sonko aliyesema kuwa, wazungu hao walikosa adabu na heshima kwa Marais wa Kiafrika
Aliyekuwa Gavana wa Nairobi Mike Sonko, hakuficha jinsi alivyokereka na hatua ya Marais wa Afrika, kulazimishwa kuabiri basi moja walipohudhuria mazishi ya Malkia wa Pili wa Uingereza.



Kwenye picha iliyozagaa mitandaoni, Rais William Ruto alionekana ameketi sako kwa bako ndani ya basi hilo, na mkewe ambaye ni Mama wa Taifa Racheal Ruto.

Picha hiyo imeonekana kumuudhi sana Sonko aliyesema kuwa, wazungu hao walikosa adabu na heshima kwa Marais wa Kiafrika.



"Hawa wazungu hawana adabu wanawekaje marais wa Africa ndani ya bus moja huko London. God forbid kitu mbaya ifanyike kwa hiyo bus itakuaje?" Sonko aliuliza kwa kushiria kuudhika.

Rais wa Tanzania Samia Suluhu, alikuwa kwenye picha hiyo iliyomwonyesha ameketi kwenye kiti cha mbele, baada ya Rais Ruto, pamoja na viongozi wengine Barani Afrika.

Siku ya Jumatatu, Septemba 19, Marais hao wa Afrika waliabiri basi hilo, lilokuwa likiwapeleka hadi Westminster Abbey, eneo ambalo mazishi ya kitaifa ya Malikia huyo wa Pili yatafanyika.

Viongozi wa mataifa ambao wanasafiri kuhudhuria mataifa hayo, walihimizwa kutumia ndege za mashirika ya kibiashara, ili kupunguza msongamano kwenye viwanja vya ndege jijini London.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad