Daktari wa Tanzania Afariki Uganda kwa Ebola

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Daktari wa Tanzania afariki Uganda kwa Ebola
DAKTARI Mtanzania aliyekuwa akisoma nchini Uganda amefariki dunia baada ya kuambukizwa virusi vya Ebola. Anakuwa daktari wa kwanza kufariki kutokana na ugonjwa huo.

-Waziri wa Afya wa Uganda Jane Ruth Ocero alitoa tangazo hilo Jumamosi kwenye ukurasa wake wa Twitter.

“Nasikitika kutangaza kuwa tumempoteza daktari wetu wa kwanza, Dk Mohammed Ali, Raia wa Tanzania, mwanaume mwenye umri wa miaka 37 leo saa 3:15 asubuhi,” aliandika.

Ocero amesema daktari huyo alifariki alipokuwa akipokea matibabu.


“Alipimwa na kuambukizwa Ebola mnamo Septemba 26, 2022, na alikufa alipokuwa akipokea matibabu katika Fort Portal RRH, kituo cha Kutengwa (JMedic).”

I regret to announce that we have lost our first doctor, Dr Mohammed Ali, a Tanzanian National, 37yr old Male today at 3:15am. He tested positive of Ebola on Sept 26, 2022 and died while receiving treatment at Fort Portal RRH, Isolation facility ( JMedic). pic.twitter.com/NoqEUtqKcM

— Dr. Jane Ruth Aceng Ocero (@JaneRuth_Aceng) October 1, 2022

Ocero akiwapa pole familia ya marehemu.

“Natoa pole kwa familia yake, madaktari, chuo kikuu cha KIU na wananchi wa Tanzania. Dk Ali ni daktari wa kwanza na mhudumu wa afya wa pili kufariki kwa ugonjwa wa Ebola. Wa kwanza alikuwa mkunga kutoka kliniki ya St Florence. alikufa kabla ya kupimwa,” alitweet.

Idadi ya watu wanaoshukiwa kuwa na Ebola inaendelea kuongezeka nchini Uganda.

Ebola ni ugonjwa mbaya na ambao mara nyingi huwa mbaya sana unaosababishwa na virusi vya Ebola.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad