Familia Wafunguka Kuhusu Picha Aliyopost Profesor Jay "Ilipostiwa Kwa Bahati Mbaya"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Saa chache zilizopita kwenye ukurasa wa Instagram wa Mkongwe wa Bongofleva Profesa Jay @professorjaytz upande wa Insta story kulipostiwa picha yake akionekana na Mke wake wakihojiwa kwenye red carpet, kitendo kilichoamsha furaha ya Mashabiki wengi kuona Mkali huyo ameimarika kiafya na wengine kuamini ameanza kuhudhuria matukio mbalimbali.

Msemaji wa Familia ya Haule @blackchatta aliyepatikana kuzungumzia hilo ameiambia AyoTV kuwa ni kweli post hiyo (ipo kwenye swipe) ilichapishwa na Profesa Jay mwenyewe lakini kwa bahati mbaya kwa sababu anatumia simu zake zote kwa sasa na huwa anaingia kwenye mitandao kuperuzi japo hajawahi kupost chochote toka January 23 2022.

“Anatumia simu zake zote sasa hivi na anaingia kwenye social media, anasoma anaona matukio yote lakini mambo ya kupost haya kwa sasa bado, anaruhusiwa kutumia simu kuangalia vitu, ile ni picha ya siku nyingi alipost kwa bahati mbaya iliteleza kwenye mikono yake lakini yuko fresh tunamshukuru Mungu”

“Watu wasiwe na hofu kama tuliyokuwa nayo mwanzo sasa hivi yupo nyumbani anaendelea na mazoezi” ——— amemalizia @blackchatta
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad