Mchungaji Awaonya Wanawake dhidi ya Kulala na Dera, Fulana: "Usilale Ukinuka Samaki"

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA




Mchungaji Rose Shaboka ameelezea kutofurahishwa kwake na wanawake wa kulala wakiwa wamevalia dera na fulana zilizoandikwa CCM akisema haziwavutii wanaume
Mtumishi huyo wa Mungu pia aliwaonya wanawake dhidi ya kufunga kanga na kuingia kitandani wakinuka samaki
Sasa anawataka wavae nguo zinazovutia kitandani na kunukia harufu nzuri kwa waume zao wapenzi
MAKINIKA: Tusaidie kubadilisha maisha ya wengi, jiunge na programu ya Patreon kutoka TUKO.co.ke.

Mchungaji maarufu nchini Tanzania amewaonya wanawake dhidi ya kuvalia dera na fulana kubwa wanapokwenda kitandani na wanaume wao.

Mchungaji Awaonya Wanake dhidi ya Kulala na Dera, Fulana: "Usilale Ukinuka Samaki"
Mchungaji Mtanzania Rose Shaboka. Picha: Rose Shaboka. Chanzo: Instagram
Mchungaji Rose Shaboka alitoa mfano wake wakati wa mahubiri ambapo alifichua kuwa alilala akiwa amevalia vazi la kuvutia akienda kitandani kisha akalivua asubuhi akija kanisani.

"Mnaziharibu t-shirt ya watu jamani. Wewe umepewa uvae kwa shughuli maalum ya chama unaenda kuilalia. Sijui nizungumze na Rais Samia Suluhu asiwape tena," alidokeza.


"Hatulali na dera sisi au tisheti zilizoandikwa CCM. Hatulali na kanga, hatulali kama tunanuka samaki," alisema Shaboka kwenye ukurasa wake wa Instagram wa Madhabau ya moto.


Pia soma
Pasta Ng'ang'a Awatahadharisha Wanaume Dhidi ya Kuwaomba Msamaha Wake Zao

MAKINIKA: Jinyakulie habari ZINAZOKUFAA ➡️ tafuta “IMEPENDEKEZWA KWA AJILI YAKO” na ufurahie!


Mtunishi huyo wa Mungu aliwashauri wanawake kuhakikisha wanapendeza na wananukia wanapokwenda kitandani na waume zao.

"Vile slay lingerie unamwachia nani, vile vinaiti dress vinavyoita bila kutoa sauti unamwachia nani?" Sahoka aliuliza.


Kwingineko, video ya mrembo akikiri kuongeza mende katika chakula cha aliyekuwa mpenzi wake iliibua gumzo mitandaoni.

Video hiyo kutoka Wasafi TV ilimuonesha dada huyo Mtanzania ambaye alikuwa kwenye mahojiano akikiri jinsi alivyokuwa akimuongezea jamaa wake nguvu za kiume.


Demu huyo alisema jamaa wake alikuwa ametekwa mno na mapenzi yake kutokana na mbinu alizotumia.

Kipusa huyo alifichua kwamba jamaa hakujua alikuwa akimpikia mende kisiri ndani ya chakula chake kumfanya awe na nguvu hata zaidi za kurina asali.

“Alinipenda sana, alinijali. Kile ambacho kilimfanya anipende hata zaidi ni jisni nilivyokuwa namtayarishia mapochopocho yani. Mimi ni mpishi Hodari. Lakini kile ambacho hakufahamu ni kwamba nilikuwa nampikia mende ndani ya chakula chake. Kabisa hilo hakufahamu,” alisema dada huyo.


Pia soma
Majambazi Wamvamia Mzee wa Miaka 70 na Kumkata Sehemu Zake za Siri


Mrembo huyo alidai kwamba mende zinaongeza nguvu za kiume. Alidokeza kwamba jamaa wake huyo alikuwa akishangaa ni vipi ikifika akati wa mechi anajikuta ana nguvu hataz zaidi.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad