Wanajeshi wa Russia wamekufa maji wakikimbia na wengine kuamua kuvaa sare za kiraia wasitambuliwe

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA



Mkaazi wa Kherson akisherekea kuingia kwa wanajeshi wa Ukraine mjini humo baada ya wanajeshi wa Russia kuondoka Nov 11, 2022
Mkaazi wa Kherson akisherekea kuingia kwa wanajeshi wa Ukraine mjini humo baada ya wanajeshi wa Russia kuondoka Nov 11, 2022
Wakaazi wa Kherson wamesherekea kuingia kwa wanajeshi wa Ukraine mjini humo na kuondoka kwa wanajeshi wa Russia.

Russia imeondoka Kherson, mji mkubwa pekee ambao wanajeshi wake walikuwa wameshikilia tangu walipovamia Ukraine mwezi Februari.

“Leo ni siku ya historia. Tunarejesha sehemu ya kusini ya nchi yetu, tunarejesha Kherson,” amesema rais wa Ukraine Volodymr Zelenskiy katika ujumbe wa video, akiongezea kwamba “kwa sasa, wanajeshi wetu wapo nje yam ji huo na karibu tunaingia katikati ya mji, lakini wanajeshi maalum tayari wameingia mjini.”

Russia imesema kwamba imeondoa wanajeshi wake 30,000 kutoka sehemu iliyo karibu na mto Dnipro, bila kupoteza mwanajeshi yeyote.


Lakini Ukraine imetoa taaswira ya wanajeshi wa Russia wakikimbia sehemu hiyo kwa haraka sana na hata kuacha nyuma sare zao, silaha na wengine kufa maji wakijaribu kujiokoa.

Wanajeshi wengine wa Russia wanaripotiwa kuvaa sare za kiraia waliposhindwa kuvuka mto Dnipro wakati wanaondoka Kherson.

Kuondoka kwa wanajeshi wa Russia katika mji wa Kherson ni mara ya tatu wanajeshi hao kuripoti kujiondoa katika ngome walizokuwa wanashikiliwa katika vita walivyoanzisha nchini Ukraine.


Jeshi la Ukraine limesema kwamba mji wa Kherson umerejeshwa chini ya udhibithi wa Ukraine na kutaka wanajeshi wa Russia waliosalia mjini humo kujisalimisha kwa wanajeshi wa Ukraine.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad