Mtoto wa Museveni Aibua Utata Mwingine

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 


Mtoto wa Rais wa Uganda, Jenerali Muhozi Kainerugaba kwa mara nyingine ameibua mjadala kupitia ukurasa wake wa wa mtandao wa kijamii wa Twitter, baada ya kutuma ujumbe wenye utata aliouambatanisha na picha ya Rais wa Rwanda, Paul Kagame.


Jenerali Kainerugaba katika ukurasa wake ameandika kuwa, ‘’Mimi ni Jenerali wa nyota 4 wa UPDF (Jeshi la Uganda), kuna vitu vichache ambavyo sijaviona katika dunia hii. Lakini ninawahurumia wale wanaomdharau mjomba wangu, Jenerali Kagame. Kupigana na Rwanda inamaanisha kupigana na Uganda!



Kauli ya Muhooozi inakuja wakati ambao mzozo kuhusu wapiganaji wa kundi la M23 na Serikali ya Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo na Rwanda na Congo inaishutumu Rwanda kuwaunga mkono waasi wa M23 walioteka maeneo mashariki mwa nchi hiyo, madai ambayo Rwanda inayakanusha.


Kwa upande mwingine inaishutumu DRC kwa kushindwa kutimiza ahadi ya kuwarejesha nyumbani waasi wa Rwanda wa kundi la FDLR walioko mashariki mwa DRC inaowashutumu kuhatarisha usalama wa Rwanda, ambapo hivi karibuni pande mbili zilirushiana maneno, kila upande ukielezea uwezekano wa kuingia vitani iwapo usalama wake utayumbishwa.

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad