Ndege ya Air Tanzania Yashikiliwa Uholanzi

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


Serikali imewatoa hofu Watanzania kuhusu taarifa za kushikiliwa kwa ndege aina ya Airbus A220 ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) nchini Uholanzi, ikisema haiwezi kutaifishwa kutokana na rufaa ya kesi inayoendelea katika Kituo cha Kimataifa cha Usuluhishi wa Migogoro ya Uwekezaji (ICSID).

Taarifa iliyotolewa na vyombo vya habari vya kimataifa viliripoti kuhusu mwekezaji wa Sweden aliyeshinda tuzo ya Dola milioni 165 (TZS bilioni 380) dhidi ya Tanzania na kuishawishi Mahakama ya Uholanzi kushikilia ndege hiyo kama kigezo cha kushinikiza malipo yake, licha ya kutopata uhalali wa ICSID.

Akizungumza na gazeti laThe Citizen, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Dkt. Eliezer Feleshi amekiri mwekezaji huyo kushinda tuzo hiyo na ndege imeshikiliwa nchini humo.

“Ni kweli kwamba walienda katika mahakama ya nchini Uholanzi baada ya sisi kufanikiwa kubishana na ICSID ili kusitisha utekelezaji, lakini kila kitu kiko chini ya udhibiti,” amesema.
-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad