Familia 20 zakumbwa na mafuriko Kinondoni

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

 



Familia zaidi ya 20 katika mtaa wa Mkunguni A kata ya Hananasifu katika manispaa ya Kinondoni nyumba zao zimeingiliwa na maji kufuatia mvua iliyonyesha leo na hivyo kulazimu familia hizo kuishi maisha ya hofu kutokana na usalama wa maisha yao kuwa hatarini


Wakizungumza nasi, familia hizo zimesema hali hiyo imewasababishia kushindwa kutoka kwenda kwenye shughuli zao za kiuchumi na hivyo kutumia muda mwingi kuchota maji yaliyoingia ndani ya nyumba zao na kuyamwaga nje huku wakieleza vyombo pamoja na vitanda vimesombwa na maji


Kwa upande wake Mwenyekiti wa serikali ya mtaa huo wa Mkunguni A Jumanne Said ameiomba serikali kuharakisha zoezi la kuwalipa fidia wananchi hao kwani walishafanyiwa tathimini na kutakiwa kuondoka

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad