Haji Manara amewatolea uvivu wale waliokuwa wanamsema beki wa Yanga SC na Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ Dickson Job kuwa ufupi wake ndio ulikuwa tatizo kwenye safu ya ulinzi ya Stars.
“Tuliambiwa wewe ni kijeba sana kucheza Central Defender, tukaambiwa ufupi wako ndio tatizo kuu kwenye safu ya ulinzi ya timu ya Taifa.
“Sijui kama kuna maswali tena kuhusu ubora wako, ilihali upo vilevile na haujaongezeka urefu hata sentimita moja.
“Top Top performance wewe na miamba wenzio pale nyuma, mechi mbili mfululizo hamjaruhusu hata goli moja mkiwazuia mastrikers warefu kama unju kwa umahiri mkubwa.
“Dickson Job muda mwingine maisha hayapo sawa bado cheki bob wa kiluguru unacheza Afrika, Maguare anazima Old Trafford.” Ameandika Haji Manara kwenye Instagram yake.
-------------------------------
Alikataa kuolewa ili amkomboe mama yake... Lakini mama ndiye aliyemuuza!
GORYANAH –Hii ni story ya Moto Sana yenye hisia na Mafunzo, binti jasiri anayepambana na siri nzito, umaskini na hatari kubwa kwa ndoto zake! Pakua app yetu ufurahie Sehemu ya 1 Hadi ya 5,na mwendelezo wake kila JUMAMOSI SAA MOJA KAMILI JIONI BURE!
Ukiona ujumbe wa allow notification bonyeza allow ili uwe mwanafamilia.