6/22/2022
Ajali ya Treni ya Abiria Leo Tabora...Mabehewa Yaanguka
Kocha Nabi Avutiwa na SIMON Msuva
SIMON Msuva yupo nchini tangu mwaka jana baada ya kuzinguana na timu yake ya Wydad Casablanca ya Morocco na kupelekana Fifa, ila juzi alifunga mabao mawili kwenye mechi ya hisani ya timu Samakiba na kuiwezesha team Kiba kubeba ubingwa wa msimu huu kwa penalti.
Mrembo Maarufu Kwenye Mitandao Poshy Queen Akana Kutengeneza Shepu Yake Matata
Poshy Queen; ni mrembo maarufu kwenye mitandao ya kijamii (sosholaiti) nchini Tanzania ambaye amekuwa akizungumziwa mno juu ya kutengeneza shepu matata aliyonayo, lakini mwenye anasema hajawahi kufanya jambo kama hiyo.
Poshy Queenn anasema kuwa umbo lake matata (kiuno cha nyigu) linatokana na asili ya familia yake kwani hata mama yake ana shepu kuliko hata yeye.
Kwa baadhi ya watu wanaojua familia ya Poshy Queen ambao ni wenyeji wa jijini Mbeya wanasema ni kweli ni asili yao kwani ndugu zake nao wamejaaliwa shepu kama ilivyo kwa wanawake walio wengi kutoka jijini Mbeya.
STOLI: SIFAE LPAUL
Chris Brown “Msinilinganishe na Michael Jackson”
Mwanamuziki Chris Brown, ameendelea kuonyesha kutoridhishwa na kundi la mashabiki pamoja na wadau wanaolinganisha umahiri wake kwenye tasnia na ule wa nguli wa Pop Hayati, Michael Jackson huku wengine wakimtaja kama msanii bora zaidi yake.
Kufuatia kukithiri kwa aina hiyo ya maoni ya watu juu ya kumlinganisha Chris Brown na Michael Jackson, mwanamuziki huyo ameamua kuvunja ukimya kwa kuweka wazi kuwa hapendezwi na aina hiyo ya maoni kutoka kwa mashabiki na wadau mbali mbali.
Breezy amesema maoni hayo ni sawa na upuuzi, likiwa ni jibu baada ya kuulizwa ni kwa namna gani huwa nachukulia suala hilo wakati akiwa kwenye mahojiano maalum na Big Boy Tv.
“Huwa najiweka mbali na mada hiyo, Maoni yangu kwenye hilo huwa ni kwamba nisingeweza hata kupumua au hata kuwa na uwezo wa kuimba kama huyu jamaa ‘Michael Jackson’ asingetokea duniani, yuko mbali sana, hakuna ushindani na yeye.” amesema Chris brown
Mgambo, ofisa mtendaji wadaiwa kuua mwanafunzi
6/21/2022
Samaki mkubwa zaidi duniani wa maji baridi avuliwa Mekong
Mwanafunzi darasa la saba auawa, adaiwa kunyofolewa macho
Gigy Money afunguka kulishana cake mdomoni na Wema
Gigy Money amejibu kuhusu gumzo lake la kulishana cake mdomoni na baadhi ya mastaa walio-show love kwenye 'Birthday Party' yake kama Wema Sepetu, Lulu Diva, Amber Lulu na Mimi Mars.
Gigy Money amesema amefanya hivyo kwa sababu stick zilikuwa zimeisha pia kitendo hicho ni ishara ya upendo
Simba SC yakanusha uvumi wa Bernard Morrison
Uongozi wa Simba SC umesema hauna taarifa zozote kuhusu Kiungo Mshambuliaji kutoka nchini Ghana Bernard Morrison kuwasilisha ombi la kutaka Barua ya Kumuachia (Release Letter), ili kumpa nafasi ya kuendelea na Maisha yake ya soka nje ya klabu hiyo ya Mismbazi.
Mwezi uliopita, Morrison alipewa ruhusa ya mapumziko na Uongozi wa Simba SC hadi mwishoni mwa msimu huu, kwa madai ya kwenda kumaliza matatizo yake ya kifamilia nchini kwao Ghana.
Mwenyekiti wa Simba SC Murtaza Magungu amesema, hawana taarifa za mchezaji huyo kuwasilisha ombi la kutaka Barua ya Kuachiwa, na wanashangazwa kuona taarifa hizo zikisambaa kwa kasi kubwa katika Mitandao ya Kijamii.
Mangungu amesema Simba SC inafahamu bado Morrison ni mchezaji wao halali, na hakuna mahala popote ambapo klabu hiyo iliwahi kuthibitisha imeachana naye.
“Morrison bado ni mchezaji wa Simba SC, tunashangazwa kuona taarifa za kutuomba Barua ya Kumuachia (Release Letter), tulimpa ruhusa ya kwenda kwao kwa ajili ya matatizo ya kifamilia,”
“Mkataba na Morrison na Simba SC bado haujakwisha, anaendelea kupata stahiki zake kama mtumishi mwingine wa klabu hii, hatujawahi kutoa taarifa popote kwamba hatutaendelea naye, na hatuna taarifa zozote za yeye kuwa kwenye mpango wa kusajiliwa na klabu nyingine.” Amesema Mwenyekiti wa Simba SC Murtaza Mangungu.
Mapema leo Jumanne (Juni 21) asubuhi, Mwandishi na Mchambuzi wa Michezo kupitia kituo cha Radio Clouds FM Shaffih Dauda alinukuliwa akisema: “Bernard Morrison anaomba release letter kwa Simba, lakini Simba hawana presha wanataka mpaka mkataba wake utamatike kisha wamkabidhi barua
Inasemekana kuna muda aliwaambia kuna klabu ya nje inamtaka, Simba wakamwambia watume offer yao watapokea ofa na watampa release letter
Taarifa za kuaminika ni kuwa anataka kujiunga na Yanga, Simba wanafahamu hilo kwahiyo hawana tatizo zaidi ya kusubiri mwisho wa mkataba”
Barbara "Simba SC Haijafeli Usajili, Tulieni Mtaona"
Afisa Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Simba SC Barbara Gonzalez amesema hadi sasa klabu hiyo imeshindwa kuipata saini ya mchezaji Victorien Adebayor aliyekua anaitumikia klabu ya USGN ya nchini Niger.
Simba SC ilijihusisha na usajili wa Mshambuliaji huyo, baada ya kuridhishwa na uwezo wake aliouonesha kwenye michuano ya Kombe la Shirikisho Barani Afrika msimu wa 2021/22.
Barbara amesema hadi sasa Simba SC haijafeli katika usajili wa mchezaji yoyote waliyemdhamiria kwa msimu ujao wa Ligi Kuu na Michuano ya Kimataifa, zaidi ya Adebayor anayedaiwa kutua kwa Mabingwa wa Kombe la Shirikisho Barani Afrika RS Berkane.
“Kumekua na taarifa nyingi kuwa tumeshindwa kuwasajili wachezaji kadhaa, sio kweli hata kidogo, tunakiri kumkosa Adebayor pekee yake, lakini kwa wengine ambao tumewadhamia tupo katika hatua nzuri za kuwasajili na watacheza Simba SC msimu ujao.”
“Simba SC inatajwa sana kwa sababu mawakala wengi wanaitumia klabu yetu kuwapandisha thamani wachezaji wao, lakini nikwambie tu tupo makini na tumeshalifahamu hilo, tunasajili kimya kimya.”
“Muda utakapofika tutawatangaza wachezaji tuliowasajili kwa ajili ya klabu yetu, Mashabiki na Wanachama waendelee kuwa watulivu, Uongozi wao upo kazini na utakamilisha kila hatua iliyoidhamiria katika usajili.” Amesema Barbara.
Simba SC imedhamiria kufanya usajili mkubwa kwa ajili ya kukiboresha kikosi chao kwa msimu ujao wa Ligi Kuu na Michuano ya Kimataifa, baada ya kushindwa kufikia lengo msimu huu 2021/22, huku ikipoteza mataji yote ya Tanzania Bara.
Zari Amzidi Kibenteni Wake Miaka 25, Wafuasi Wake Wampinga, Awajibu Kuwa…
Yanga Yashauriwa Kutoa Milioni 20 Kukamilisha Usajili wa Morrison Kutoka Simba SC
Ole Sabaya Aivaa Takukuru Akisema ‘Gerezani si Pikiniki’
Habari za Ndani Kabisa Zinasema Simba Wagoma Kumpa Release Letter Bernard Morrison
Bernard Morrison anaomba release letter kwa Simba, lakini Simba hawana presha wanataka mpaka mkataba wake utamatike kisha wamkabidhi barua
Inasemekana kuna muda aliwaambia kuna klabu ya nje inamtaka, Simba wakamwambia watume offer yao watapokea ofa na watampa release letter
Taarifa za kuaminika ni kuwa anataka kujiunga na Yanga, Simba wanafahamu hilo kwahiyo hawana tatizo zaidi ya kusubiri mwisho wa mkataba
Mbosso ‘Afunguka’ Kuwa na Maradhi ya Moyo
Mwanamuziki mahiri wa Bongo fleva, Mbwana Yusuf Kilungi maarufu Mbosso amefunguka juu ya kupambana na ugonjwa wa moyo, unaodaiwa kusababishwa na maumbile ya kuzaliwa.
Akizungumza na kipindi cha Fresh mwisho wa juma lililopita, Mbosso amesema amekuwa akipambana na ugonjwa huo kimya kimya na kuwajulisha watu wachache tu wa karibu yake.
Mbosso ameweka wazi kuwa wakati mwingine hupitia wakati mgumu kutokana na kuwa usingizi na wakati mwingine hupata maumivu ya mwili kupita kiasi.
“Ndiyo nina matatizo makubwa ya moyo lakini namshukuru Mungu naendelea vizuri, nafanya mazoezi ya viungo mara kwa mara ili kudhibiti hali hiyo lakini wakati mwingine napata shida hata kufanya mazoezi kwa vile nina maumivu,” amesema Mbosso.
Huku akibainisha kutopenda kuongelea chochote kuhusu masuala yake binafsi, lakini amesema tayari amewajulisha baadhi ya wanafamilia, watu wake wa karibu na mabosi wake akiwamo msanii Diamond Platnumz juu ya tatizo linalomsibu.
“Bosi wangu mmoja alikuwa anajua, mama yangu pia anafahamu hali hiyo na pia nilimjulisha Diamond pamoja na wazazi wenzangu ila binafsi huwa sizungumzii mambo yangu binafsi mara kwa mara,” aliongeza.
Aidha, Mbosso ameweka wazi kuwa daktari aliyemfanyia uchunguzi amebaini kuwepo kwa mafuta mengi mwilini kwake ambayo yameziba sehemu ya mishipa ya damu hali inayopelekea wakati mwingine kukumbwa na tatizo la kutetemeka.
Mwimbaji huyo amesema kwamba yuko tayari kusafiri kwa ajili ya matibabu ambayo ilikuwa ayafanye muda mrefu lakini alichagua kusubiri ili kuweka mambo sawa na kuiacha familia yake katika hali nzuri kwakuwa matibabu hayo yatachukua muda mrefu.
Ugonjwa anaougua Mbosso unajulikana kwa jina la Atherosclerosis, ukiwa ni wa hali ya kawaida ambao hutokea wakati dutu nata iitwayo plaque kujilimbikiza ndani ya mishipa na uundaji wa plaque huzuia mtiririko wa damu kuenea vizuri kwenye viungo vya mwili na tishu.
Maumivu ya kifua na upungufu wa kupumua ni dalili za kawaida za hali hiyo ambayo madaktari wanasema husababishwa na ulaji wa juu wa cholesterol, shinikizo la damu na kuvuta sigara.
Viwanja vikubwa Vinauzwa: Bunju na Mapinga
Harmonize Apagawa na WIMBO wa Sarafina "Upo Nyonyo" Kisa Kajala Masanja
'Real Recognize Real' hivyo ndivyo unavyoweza kusema, hii ni baada ya mwimbaji @saraphina__tz kumshukuru @harmonize_tz kwa kusapoti wimbo wake mpya uitwao "UPO NYONYO" kwa kujirekodi akiimba wimbo huo.
"Y’aaaaaaallll 🙌🏻🙌🏻🙌🏻🙌🏻 @harmonize_tz , thank you so much for your support 😩😩😩😩😩 🙌🏻🙌🏻 bless u 🙏" ameandika Saraphina kupitia ukurasa wake wa Instagram.
@harmonize_tz alishare kipande cha video akiiambia wimbo wa Saraphina kupitia insta story yake akiwa na Dj wake, Dj Seven na kuisindikiza na maneno kuwa wimbo huo mpenzi wake @kajalafrida anaupenda sana mpaka amesababisha na yeye aupende.
"My woman love this song (Upo Nyonyo) kila siku. Yoo is a banger, nasikiliza all night. Ukirudi (Kajala) utanikuta nishaishika Upo Nyonyo. Someone tell Queen Fina, this is another anthem @saraphina__tz " - ameandika Harmonize.
"Upo Nyonyo" ni wimbo wa TATU kwa Saraphina kuuachia mwaka 2022, na umapata mapokezi makubwa kwa mashabiki wake. Nyimbo zake nyingine ni pamoja na "Wamerudiana" na "Number One" alizoziachia mapema mwaka huu
Wanafunzi 4 Wafariki Baada ya Ajali ya Boda Boda na Lori Mapinga, Mwanafunzi Aliekuwa Anaendesha Boda Aliwabeba Mshikaki Wenzake Watatu
Wanafunzi wanne wamefariki Dunia baada ya pikipiki waliyokuwa wakisafiria kugongwa na Lori, katika kitongoji cha Kihara kata ya Mapinga wilaya ya Bagamoyo, mkoani Pwani.
Akizungumza na TimesDigital mwenyekiti wa Kitongoji cha Kihara Simon Kilian amesema, ajali hiyo ilitokea juzi jioni ambapo Pikipiki iliyokuwa ikiendeshwa na mmoja wa wanafunzi hao, iligonga kingo ya Barabara na Wanafunzi hao kuangukia barabarani hali iliyosababisha kukanyagwa na lori hilo.
“Wanafunzi walipoangukia Barabarani Lori lilikuwa katika mwendo kasi na kuwakanyaga, na hawa wanafunzi waliweza kutambulika kwa sababu mmoja aliazima Pikipiki ndipo mwenye Pikipiki akawajulisha wazazi wa wanafunzi hao.” Alisema Kilian.
Mwenyekiti Kihara amesema mara baada ya tukio hilo miili ya wanafunzi hao ilipelekwa kituo cha afya Karage, na baadae wazazi walifika ili kuitambua miili hiyo, baada ya wazazi kuitambua miili ya watoto wao ililazimika kuwazika kutokana na hali zao kuwa mbaya.
Katika hatua nyengine Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani, Gregory Mushi amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo.
Nicola Traldi akamatwa kwa kumshambulia na kumjeruhi mpenzi wake Miss Chanty (EX wa Eric Omondi)
Nicola Traldi akamatwa kwa kumshambulia na kumjeruhi mpenzi wake Miss Chanty (ex wa Eric Omondi)
VIDEO: