Wanakijiji Wauza Figo zao Wakidanganywa Zitaota tena

Wanakijiji Wauza Figo zao Wakidanganywa Zitaota tena


Baadhi ya wanakijiji cha Hokse huko nchini Nepal wamekuwa wakirubuniwa kuuza figo zao huku wakidanganywa kuwa zitaota nyingine.


Kijiji hicho miaka kadhaa nyuma kilikuwa maarufu kama 'Kijiji cha Figo' kwa sababu kila nyumba ilikuwa haikosi mtu aliyeuza figo (mwenye figo moja).


Madalali wamekuwa wakizunguka kila kona ya kijiji hicho wakiwalaghai wananchi wauze fio zao japo kwasasa ni kosa la kisheria kufanya hivyo.


Baadhi yao wamekuwa wakilalamika kuwa walidanganywa kuwa figo zao zitaota tena na wengine wamepoteza baada ya kutolewa figo hizo kienyeji.

Post a Comment

0 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad

Below Post Ad