AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Jana, TFF na Azam Media zilisaini mkataba huo wa miaka mitatu utakaogharimu Sh5.6 bilioni, ambapo zitalipwa kwa vipindi vitatu.
Awali, pande hizo mbili ziliingia mkataba wa makubaliano kabla ya jana kusaini mkataba rasmi.
Katika mkataba huo, kila klabu itaweka kibindoni kitita cha Sh100 milioni kutoka Azam Media, ambayo itakuwa inaonyesha ‘Live’ mechi za Ligi Kuu kupitia Azam TV.
Hata hivyo, mkataba wa makubaliano kati ya Azam Media na TFF ulipingwa na klabu ya Yanga, ambayo ilidai ulikuwa na upungufu na kuomba upitiwe upya kabla ya kusainiwa mkataba rasmi.
Akizungumza wakati wa hafla ya kusaini mkataba huo, Makamu wa Pili wa Rais wa TFF, Athuman Nyamlani alisema, fedha zitakazotolewa na Azam Media zitazisaidia klabu kutekeleza mipango ya maendeleo.
“Soka haliwezi kuendeshwa kwa viingilio, mkataba huu utazisaidia klabu kutekeleza mipango ya maendeleo sambamba na kuifanya ligi yetu iwe bora,” alisema Nyamlani.
Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrence Mwalusako alisema ameshangazwa na uamuzi wa Azam Media na TFF kusaini mkataba wakati mapendekezo yao hayajafanyiwa kazi.
“Taarifa za kusaini mkataba nimezisikia leo asubuhi, kweli zimenishangaza. Makubaliano yalikuwa, bodi ya Ligi na Azam ziupitie upya kisha mwanasheria wetu auone ndiyo mambo mengine yafuate,” alisema Mwalusako.
Aliongeza: “Siwezi kulizungumzia sana hili, lakini ndiyo yalikuwa makubaliano yetu sasa kama wamesaini bila mapendekezo yetu kufanyiwa kazi ni jambo linaloshtua.”
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Yanga hamna jipya kaaeni pembeni wacha ligi ye2 ya bongo iende mbele iwe km ulaya
ReplyDeleteKauzee zeni ndala ligi ishawashindaaa
ReplyDelete