Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji Tanzania (Ewura) imetangaza kuanza kutumika kwa bei mpya za mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa kuanzia leo Jumatano Mei 4, 2022 ambapo bei ya nishati hiyo imeendelea kuongezeka.
5/04/2022
Bei Mpya za Mafuta ya Gari Zilizoanza Kutumika Leo Hizi Hapa
Mamlaka ya Udhibiti wa Nishati na Maji Tanzania (Ewura) imetangaza kuanza kutumika kwa bei mpya za mafuta ya petroli, dizeli na mafuta ya taa kuanzia leo Jumatano Mei 4, 2022 ambapo bei ya nishati hiyo imeendelea kuongezeka.
10/03/2021
5/25/2021
Tanzania yaweka rekodi mauzo ya dhahabu
4/11/2021
Mashahidi 18 kutoa ushahidi kesi ya kusafirisha kilo 19 za heroin
2/03/2021
Petroli, Dizeli Bei Juu
1/23/2021
Shilingi Trilioni 18 zinapita kwenye huduma ya fedha mtandao kwa mwezi
8/05/2020
Ndege Kubwa Kubwa za Kimataifa Zaendelea Kutua Tanzania Licha ya Corona Kuitesa Dunia
Unazoziona ni Baadhi ya ndege kubwa kama zilivyokutwa leo katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere Jijini Dar es salaam.
7/31/2020
Masoko ya Hisa Duniani Yaporomoka
Masoko ya hisa duniani na masoko ya hisa nchini Marekani yamelegalega baada ya hazina ya Marekani kuonya kwamba janga la virusi vya corona huenda likatishia uchumi uliorejea katika hali ya kawaida uliyoweka viwango vya riba karibu ya sifuri.
Kuanguka kwa hisa kuliongezeka kwa kasi katika mataifa ya Ulaya baada ya Ujerumani kusema uchumi wake ulinywea kwa asilimia 10 katika robo ya pili kwenye kipindi cha miezi mitatu iliyopita. Viwango vya chini vya riba na matarajio ya wawekezaji juu ya uwezekano wa kupatikana kwa chanjo dhidi ya virusi vya corona vilisaidia masoko ya dunia kuwa kwenye hali nzuri katika sehemu kubwa ya mwaka huu.
China na Urusi Zawekewa Vikwazo na Umoja wa Ulaya
Umoja wa Ulaya umeziwekea China, Urusi na Korea Kaskazini vikwazo kwa kuwapiga marufuku maafisa wa idara za ujasusi za nchi hizo kuingia katika nchi za Umoja wa Ulaya. Umoja wa Ulaya umechukua hatua hiyo kutokana na idara hizo kutuhumiwa kushiriki katika shughuli za udukuzi wa kimtandao duniani kote.
Idara hizo za ujasusi zinatuhumiwa kujaribu kufanya udukuzi kwenye shirika la kudhibiti silaha za nyuklia. Waliowekewa vikwazo hiyvo ni maafisa sita na taasisi kadhaa za nchi hizo tatu.
Na kwa ajili ya kujihami dhidi ya hujuma za kimtandao Umoja wa Ulaya ulipitisha utaratibu wa kisheria wa kuuwezesha kuweka vikwazo. Vikwazo vya Umoja wa Ulaya pia vitahusu kuzuia mali za watu na hata za taasisi.
7/30/2020
Mahakama Manyara yataifisha Madini ya Tanzanite yaliyokamatwa Simanjiro
Julai 29,2020, Mahakama mkoani Manyara imeyataifisha Madini ya Tanzanite gramu 132.64 yenye thamani ya shilingi Milioni 18,446,894.14 yaliyokutwa kwa mfanyabiashara wilayani Simanjiro Mkoa wa Manyara, kinyume na Sheria.
Mfanyabiashara huyo wa madini ya Tanzanite wilayani humo Lucas Liaseki amekamatwa na kufikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa Manyara mbele ya hakimu mkazi Simon Kobelo baada ya kujaribu kutorosha madini ya Tanzanite katika geti la ukaguzi wa madini hayo Mirerani.
Wakili wa serikali mwandamizi ambaye pia ni mkuu wa mashtaka mkoa wa Manyara Mutalemwa Kishenyi amesema mfanya bishara huyo alikamatwa kwa kosa la kutokuwa na kibali cha ambapo serikali imeyataifisha.
Aidha amesema mahakama imetoa adhabu ya kifungo cha nje cha miezi 12 na kumuamuru asifanye kosa lolote kwa kipindi hicho.
7/01/2020
Kimenuka..Kampuni ya Moil Yalipa Faini ya Tsh Milioni 10 Kwa Kuhujumu Mafuta
6/05/2020
Shirika la ndege la Qatar kuanza safari Nchini Tanzania
6/01/2020
PICHA: Muonekano wa Barabara za juu Ubungo, Vyombo vya Usafiri vyaanza Kupita
Ni Mei 30, 2020 ambapo Barabara za juu (Flyover ) iliyojengwa Ubungo Dar es Salaam imeanza kufanya kazi ambapo vyombo vy usafiri vimeruhusiwa kupitia, hapa nimekusogezea picha 11 ujionee.
5/30/2020
Abiria 200 Wasafiri Kutoka Tanzania Kwenda India Kwa Air Tanzania
5/24/2020
Habari Njema....Ndege ya Kwanza ya Watalii Yatua Uwanja wa Ndege ya Kia
5/19/2020
Serikali Yatangaza Utaratibu Mpya Kwa Watalii “Hawarudi Nyumbani Mwezi Mmoja”
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Mhandisi Isack Kamwelwe, ametangaza kufunguliwa kwa anga la Ndege la Tanzania, ambapo kwa sasa Ndege za Kitalii, na kibiashara zitaruhusiwa kuingia nchini.
Aidha ameitaka ATCL kujipanga ili kurejesha huduma za usafiri.
Wakati huohuo akizungumza Jijini Dodoma, Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt.Hamis Kigwangalla amesema kuanzia sasa watalii wanaruhusiwa kuingia nchini na kupimwa.
Dr. Kigwangalla amesema katika zoezi hilo wahudumu wa Viwanja vya Ndege, pamoja na wahudumu wa watalii watalazimika kupimwa Corona kila mara pindi wanapoingia Tanzania.
Aidha Waziri Kigwangalla amesema, Wizara ya Uchukuzi kwa kushirikiana na Wizara ya Afya, zitasimamia miongozo maalumu iliyowekwa ikiwamo kufungua anga ili kuruhusu ndege zianze kuingia.
5/16/2020
Habari Njema Kwa Watanzania..PATO la Taifa Lapanda kwa Asilimia 7
Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philip Mpango amesema pato la taifa limekuwa kwa asilimia 7 kwa mwaka 2019 sawa na ilivyokuwa kwa mwaka 2018.
Dkt. Mpango ameyasema hayo Bungeni mjini Dodoma wakati akiwasilisha makadirio ya bajeti kwa mwaka wa fedha 2020/2021 na kueleza sekta ambazo zinaongoza kwa ukuaji nchini.
Amezitaja sekta zilizoongoza katika ukuaji ni pamoja na uchimbaji wa madini na mawe kwa asilimia 17.7, ujenzi kwa asilimia 14.1, sanaa na burudani asilimia 11.2, usafirishaji na uhifadhi wa mizigo asilimia 8.7.
Katika hatua nyingine Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai aliikataa hotuba ya bajeti ya fedha na mipango ya kambi ya upinzani kutokana na Waziri Kivuli Mh. Halima Mdee kutokuwepo bungeni wakati baadhi ya wabunge waliokuwa wamejiweka karantini wamerejea bungeni.
5/13/2020
Wafanyabiashara Simiyu Wakubali Kuuza Sukari 1,900
Wafanyabiashara wa sukari Wilaya ya Bariadi, Mkoa wa Simiyu, wametangaza kushusha bei ya bidhaa hiyo kutoka Sh 3,200 kwa kilo moja ilivyokuwa ikiuzwa awali, hadi Sh 1,900, ili kutii maagizo ya Serikali.
Sukari
Hatua hiyo imekuja kufuatia kikao cha pamoja, baina ya wafanyabiashara wa sukari wa rejareja na jumla na Mkuu wa Wilaya ya Bariadi, Festo Kiswaga, kikicholenga kujadili mstakabari wa bei ya bidhaa hiyo.
Katika kikao hicho, Serikali ilisema kuanzia leo Jumanne, itaanza kuwakamata wafanyabiashara watakaobainika kuuza sukari juu ya Sh 1,900, ambayo ni bei elekezi ya mamlaka, na hii ndiyo kauli za Serikali.
5/09/2020
Serikali Itumie Mdororo wa Bei ya Mafuta Duniani Kuwekea Akiba
4/21/2020
Bei ya Mafuta Yashuka....
Bei ya mafuta imeshuka kwa kiwango kikubwa ambacho hakijawahi kuonekana kwa zaidi ya miongo miwili wakati wafanyabiashara wakizidi kuingiwa na wasiwasi kwamba hifadhi zao zinaelekea kufikia kikomo.
Dalili zinazonesha kwamba nchi za Ulaya na Marekani ambazo zimezongwa na janga la virusi vya Corona huenda zimeshindwa kuzisaidia hisa za nchi za Asia kuongeza viwango vyao vya bei za hivi karibuni.
Wachambuzi wanasema hatua ya makubaliano yaliyofikiwa mwezi huu kati ya wazalishaji wakuu wa mafuta duniani ya kupunguza uzalishaji kwa mapipa milioni 10 kwa siku imeleta matokeo machache katika mgogoro wa mafuta kutokana na kuwepo hatua za nchi kufunga shughuli za kibiashara pamoja na kusimama kwa safari za ndege, hatua ambazo zimewafanya mabilioni ya watu kubakia majumbani.