Lupita Nyong’o Athibitisha Kuwa na Hhusiano wa Kimapenzi na Rapa Huyu.

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Lupita amezidi kuchukua headlines za vyombo mbalimbali vya habari tangu afanikiwe kuchukua tuzo za Oscar na kutajwa kama mwanamke mrembo zaidi duniani, sasa amethibitisha kuhusu upande wake wa mahusiano kuwa ni kweli ana uhusiano wa kimapenzi na mwanamuziki K’naan kutoka Somalia.

Mara ya kwanza Lupita alikuwa akihusishwa na Michael Fassbender na Jared Leto lakini mwigizaji huyo amekita mizizi yake ya kimapenzi kwa rapa K’naan na wanafuraha na mahusiano yao.
Wapenzi hao mara kadhaa wamekuwa wakionekana katika maeneo mbalimbali wakiwa pamoja lakini hawakuwa wakiweka wazi nini kinaendelea kati yao na kufanya watu wahisi tu juu ya uhusiano wao.

Stori ni kwamba katika jarida la hivi karibuni la Vogue ambalo Lupita ametokea kwenye ukurasa wa mbele amethibitisha kweli ana uhusiano wa kimapenzi na K’naan na anampenda sana.
K’naan ni mzaliwa wa Somalia na ameingia katika umaarufu baada ya kuimba wimbo rasmi wa kombe la dunia kwa mwaka 2010 wa “Wavin’ Flag”.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. haina shida ni mkubwa anaweza kuamua chochote ktk maisha, kila la kheri ktk mpnz yenu

    ReplyDelete

Top Post Ad