Malawi Wameanza Chokochoko Ndege yao Yaonekana Ikifanya Doria Ileje, Wananchi Wataaruki

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

MBUNGE wa Ileje, Aliko Kibona (CCM) ameomba Serikali ieleze juu ya ndege kutoka Malawi, ambayo imekuwa ikitia hofu wananchi wa Ileje, kwa kuzunguka angani kila mara.

Mbunge huyo alisimama kutoa hoja hiyo baada ya kipindi cha maswali na majibu na kuomba mwongozo wa Spika, Anne Makinda kuhusu suala hilo. Kibona alisema:

“Nazungumzia jambo mahsusi linalotokea katika mpaka wa Tanzania na Malawi katika Jimbo la Ileje. Kwa sasa kuna ndege kutoka nchi ya Malawi inazunguka katika vijiji jirani na tayari imeleta hofu kwa wananchi; na watoto hawawezi kusoma. Ninaomba mwongozo wako kama nipo sahihi. Naitaka Serikali kwanza ieleze ile ndege inatoka wapi na inafanya nini; na Pili naitaka Serikali imfahamishe Mkuu wa Wilaya ya Ileje kuhusu ndege hiyo ili naye awafahamishe wananchi ili wasiwe na hofu”.

Mbunge huyo alisema aliamua kuleta hoja hiyo bungeni, kwa kuzingatia uhusiano uliopo hivi sasa baina ya Tanzania na Malawi. Baada ya maelezo hayo ya Kibona, Spika alisema:

“Suala la Mheshimiwa Kibona linahitaji kufanyiwa kazi sana”. Serikali inaendelea na vikao vyake na itampatia majibu Kibona baada ya kutafakari na kujadili suala hilo.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

8 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. Wanaanza uchokozi,sijui ni laana ya kukubaliana na ndoa za jinsia moja ndio inaanza.

    ReplyDelete
  2. Hawana lolote waache waanze porojo zao tuwachakaze vizur kiinchi chenyewe ni kama kibiriti tu, alafu duh huyo rais wao kiumbe cha ajabu na sura yake ni nzito kweli

    ReplyDelete
  3. Vita mnaijuaa au mnaona kwenye tv?

    ReplyDelete
    Replies
    1. Tunaijua lakin sio kwa ki nchi kama malawi kuanza kututishia na wakati tukisema hakuna kupitisha vitu kwenye bandari yetu uchumi wao utashuka mafuta na vitu kibao wanapitisha kwetu nchi yenyewe njaa tu we si unaona wanakuja huku kuwa ma house boy tu!kunamtanzania ataenda malawi kufanya kazi za ndani?

      Delete
    2. Nimekupenda buree kwani bahari tsh ngapi nikununulie...lazima ujiamini hata adui akuogope tutawachakaza asubuhi hadi saa 4 mchana tumemaliza vita tunafurahia ushindi...watulie nchi yenyewe masikini badala wafanye yao kutwa kuchokonoa ya wenzao..mungu wanusuru waamke usingizini kuinua uchumi wao..

      Delete
  4. aache ubwege huyo mutiririka hapo kwnye zizi lake la ng'ombe!

    ReplyDelete
  5. apewe CD ya maazimisho ya miaka 50 ya muungano aione kwanza kabla hatuja vuka mpaka kuelekea kunako.

    ReplyDelete
  6. Anatafuta misifa tz inavijana wa kazi wa kutosha!Naona hajui kma sisi tunamchango mkubwa sana ktk ukombozi wa nchi za kusini mwa afrika!

    ReplyDelete

Top Post Ad