Miujiza: Mwanamke Ajifungua Baada ya Kuwa Mjamzito kwa Miaka 14

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mwanamke wa Nigeria aliyejitambulisha kwa jina la Mercy James amesimulia tukio la ajabu la kujifungua salama mtoto wa kike baada ya kuwa mjamzito kwa kipindi cha miaka 14. Mtoto aliyeamua kumuita ‘Miracle’

Kwa mujibu wa Vanguard, Mercy alieleza kuwa alianza kujisikia dalili za ujauzito miaka 14 iliyopita lakini awali dalili hizo zilikuwa zinabadilika na mara nyingine anaingia katika hedhi kwa siku moja, lakini hali ilianza kuwa serious miaka miwili baadae alipoenda hospitali na kuhakikishiwa kwa vipimo kuwa ni mjamzito.

“Nilienda tena kwa tabibu miaka miwili baadae na kumlalamikia kuhusu maumivu niliyokuwa nayapata, aliniambia tena kuwa sina tatizo la tumbo na kwamba huo ulikuwa ujauzito. Alinishauri niendelee na maombi ili Mungu aniepushe na mikono ya shetani.” Mercy alisimulia.

Anaeleza kuwa alikuwa anatumia madawa mengi ya kutibu magonjwa ya tumbo lakini hali yake haikubadilika.

Hali iliendelea hivyo hadi ilipofika June 7 mwaka huu ambapo alienda tena katika hospitali hiyo akiwa analalamika na kusikia kila dalili za kitu kutaka kutoka mwilini mwake, lakini hakufahamu kuwa hiyo ingekuwa siku ambayo angejifungua mwanae wa kike, ‘Miracle’.

“Kisha Mungu aliamua kunifuta machozi. Katika siku niliyojifungua mwanangu wa kike, mwanzo nilihisi ni minyoo inataka kutoka kwenye mwili wangu bila kufahamu kuwa yule alikuwa mtoto. Hivi ndivyo nilivyomwambia mkunga. Lakini baada ya kunipima alianza kuniambia nisukume. Nilimpotezea. Baadae nikaishiwa fahamu kama dakika 15 na nilipopata fahamu, nilisikia mtoto Analia. Nilishangaa sana na kuchanganyikiwa nilipomuona mwanangu. Sikuweza kuamini macho yangu.” Mercy aliendelea kusimulia tukio hilo.

Naye tabibu wa hospitali ya kanisa la ‘Celestial Church Of Christ, Parokia ya Kadoso ambapo Mercy alijifungulia, aliyetajwa kwa jina la Ajegunle aliliambia Vanguard kuhusu hatua zote alizopitia hadi kujifungua mwanae huyo na jinsi yeye binafsi kama mkunga alivyohusika.

Marafiki na ndugu wa mwanamke huyo walitoa ushuhuda pia kwa gazeti la Vanguard la Nigeria kuhusu tukio hilo la kushangaza.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. da kweli hii ni miujiz ya mungu, nina ushuhuda kuwa nina dada yangu anamimba ina miaka nane sasa ilikuwa ikipotea na kuonekana, kupotea na kuonekana na sijui atajifungua lini yailah, na ana blidi kila mwezi

    ReplyDelete

Top Post Ad