Sumaye: Rushwa ikizidi CCM Hakika Nitajiondoa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Waziri Mkuu mstaafu, Fredrick Sumaye amesema iwapo misingi ya uchaguzi ndani ya CCM italalia kwenye rushwa, hataendelea kuwa mwanachama na kuonya kuwa tatizo hilo limefikia pabaya na litakiangusha chama hicho.

Sumaye, ambaye alipewa adhabu ya kudhibitiwa kwa miezi 12 kwa kosa la kuanza kampeni za urais mapema, alisema msimamo wake wa kupinga rushwa na tabia yake ya kujishirikisha kwenye mambo ya kijamii vinaweza kuwa sababu ya kutuhumiwa kufanya kampeni na baadaye kupata adhabu hiyo.

Alionya kuwa vurugu zinazotokea sasa, hasa kwenye mikoa ya Kusini si ajali, bali hasira za wananchi dhidi ya viongozi wao ambao alisema wamejitenga baada ya kupata madaraka na hivyo wananchi wanatumia kila nafasi wanayoipata kuwaadhibu.

Katika mahojiano maalumu na waandishi wa gazeti hili, Sumaye ambaye alijitokeza kwenye kinyang’anyiro cha urais mwaka 2005 lakini hakupitishwa na CCM, alisema hawezi kuendelea kuwamo kwenye chama endapo kitachagua viongozi kwa rushwa.

“Suala si kama mimi nagombea au sigombei… Hata kama sigombei. Kama nitajiridhisha mwenyewe kuwa huyu amefika pale (amechaguliwa) kwa sababu ya rushwa, sitakuwapo sehemu hiyo (kwenye chama hicho), hata kama sigombei,” alisema Sumaye katika mahojiano hayo yaliyofanyika nyumbani kwake Kiluvya, takribani kilomita 30 kutoka jijini Dar es Salaam.

Sumaye, ambaye ndiye waziri mkuu pekee aliyemaliza awamu mbili za jumla ya miaka 10 bila ya kuondolewa, alikuwa akijibu maswali kuhusu mustakabali wake ndani ya CCM ambayo anadai imetawaliwa na rushwa. Maswali hayo na majibu yake yalikuwa:

Waandishi: Mwanzo ulisema rushwa inapokithiri kuna watu wanaweza wakatoka kwenye chama. Inavyoonekana katika mazungumzo yetu haya, wewe ni mtu ambaye unaichukia sana rushwa. Unafikiri, hivi (rushwa) inavyoendelea na labda kwenye uchaguzi wa mwakani itakuwa hivyo, unaweza siku moja ukatoka CCM?

Sumaye: Hilo nafikiri nilishawahi kulisema… nilisema kama misingi ya uchaguzi kwenye Chama Cha Mapinduzi italalia kwenye rushwa, mimi sitakuwa sehemu ya hiyo. Hilo nilishalisema na wala sibahatishi. Sasa suala si kama mimi nagombea au sigombei, hata kama sigombei. Lakini… kama nitajiridhisha mwenyewe kuwa huyu amefika pale (amechaguliwa) kwa sababu ya rushwa, sitakuwapo sehemu hiyo. Hata kama sigombei.

Waandishi: Utakuwa radhi kusema sipo mahali hapa?

Sumaye: Sasa kama naweza kusema sasa, unataka nisemeje? niandike kwa damu? (anacheka).

Sumaye, ambaye alishindwa kwenye uchaguzi wa wajumbe wa Nec mwaka 2012 kwenye Wilaya yake ya Hanan’g, alisema nchi imefika mahali pabaya kiasi kwamba watu wanaona wakati wa uchaguzi ndiyo halali kwao kupokea rushwa.

“Unajua, imefika mahali watu hawawezi kujitokeza kwa sababu inaonekana mazingira yanayotakiwa ni ya rushwa. Kwa hiyo anasema ah, ya nini? Hata usiende kwenye ngazi ya urais, hivi unadhani hakuna watu wazuri ambao wangekuwa wabunge? Wako,” alisema mbunge huyo wa zamani wa Hanang na kuongeza:
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

1 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.

Top Post Ad