Lissu: Marehemu Amepiga Kura Katiba ya Sitta

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA


MWANASHERIA wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Tundu Lissu amesema mchakato wa kutengeneza katiba mpya ni wa kihistoria kwani jina la marehemu lilipiga kura.

Akifafanua kauli hiyo alisema jina la mjumbe Shida Salum aliyefariki dunia Julai mwaka huu, limo kwenye orodha ya waliopiga kura ya ndiyo wakati kupitisha Katiba inayopendekezwa.

Lissu alisema hayo mwishoni mwa wiki mjini hapa alipotoa mada kwenye mdahalo wa kujadili Katiba iliyopendekezwa inayosubiri kupigiwa kura na wananchi, ambako alihoji ni Katiba Mpya au katiba ya kiimla katika rangi ing’aayo.

“Aliyekuwa mjumbe wa Bunge Maalum la Katiba kundi la 201 kila mmoja anajua kwamba alifariki dunia lakini ukiangalia kwenye orodha ya waliopiga kura (huku akiionyesha kitabu kwa washiriki), anaonekana amepiga kura ya ndiyo.

“…Hii inawezekanaje jamani, ndiyo maana nakubaliana na Rais (Jakaya Kikwete) kuwa hii katiba iliyopendekezwa ni ya kihistoria,” alisema Lissu ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA.

Mwanasheria huyo ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki, alisema kitendo cha baadhi ya wajumbe kupiga kura wakiwa hospitalini ni miongoni mwa matukio yatakayokumbukwa kwa kuweka historia kwani halijawahi kutokea sehemu yoyote ulimwenguni.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Tags

Post a Comment

2 Comments
* Please Don't Spam Here. All the Comments are Reviewed by Admin.
  1. CCM are capable of doing anything jus to get what they want............fkthm

    ReplyDelete
  2. hiiii ni hatari, wanafanya masihara mpaka kwa watu waliokufa? tena ningekuwa Zito Kabwe ingekuwa shidaaa, maanake huyo Shida salum ni mama yake mzazi.

    ReplyDelete

Top Post Ad