AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Askofu msaidizi wa jimbo hilo, Eusebius Nzigilwa, alisema kitendo hicho ni cha kipagani na kamwe Watanzania wanapaswa kuwaepuka kama ukoma wagombea wa namna hiyo na wale watakatumia fedha kama ushawishi wa kuwachagua.
Askofu Nzigilwa alitoa kauli hiyo jana wakati akihubiri katika sherehe ya upadrisho wa Padri Tito Rwegoshora na mafrateli watatu kupewa daraja la ushemasi.
Alisema ni jukumu la Watanzania kuliombea taifa liepukane na roho ya kipagani kwa wagombea dhidi ya Watanzania wengine wakati wa mchakato wa uchaguzi Mkuu.
“Mwaka huu tunaingia katika uchaguzi mkuu, wa kumchagua rais, wabunge na madiwani, hivyo Watanzania tunapaswa kuwa makini n kwa kuliombea Taifa,” alisema.
“Sitabiri vifo, jitokezeni kwenda kugombea, ila msiende huko kufanya upinzani wa ‘makafara’ wagombea wenzenu kama Herode alivyowaua wazaliwa wa kwanza wa kiume,” alisema.
Alisisitiza kuwa viongozi watoa rushwa na wale wanaoangamiza wagombea wenzao wasichaguliwe kwa kuwa maangamizi na rushwa vinakiuka maadili ya uangozi bora.
Aidha, Askofu Nzigilwa alisema kuwa Herode alishukuru kuzawili kwa Yesu Kristo kisiasa, moyoni mwake alihofia kuzaliwa kwa mfalme wa wayahudi kungeleta mapinduzi katika uongozi wake.
“Roho ya Herode ya kuua watu tunaziona hadi leo, sisi tunaomtafuta Yesu sasa tujiulize tunakwenda kwa Yesu kumsujudia au kumwangamiza,” alisema.
Aliwaonya waliopata upadirisho na ushemasi kutotumikia mabwana wawili, anasa na Mungu, bali wanapaswa kutumikia wito wao wa kichungaji.
CHANZO: NIPASHE
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Halafu hawa Maaskofu Wanga,Mimi kanisa nimemalizana nalo
ReplyDelete