AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA
Mkuu wa Idara ya Habari na Mawasiliano ya Yanga SC, Jerry Muro amewaambia Waandishi wa Habari leo katika hoteli ya Zanzibar Ocean View visiwani hapa kwamba, hatua hiyo imefikiwa baada ya mchezaji huyo kuanza kujiengua katika timu.
“Tumefikia uamuzi wa kuachana na Kaseja, baada ya yeye mwenyewe kuanza kujiengua katika timu,”amesema Muro.
Mwishoni mwa mwaka jana, Kaseja aliwasilisha barua kwa mwajiri wake, Yanga SC kutoa taarifa ya kuvunja makataba wake, uliokuwa umebakiza mwaka mmoja.
Katika barua yake, Kaseja alisema sababu ya kuvunjwa Mkataba huo ni kukiukwa kwa masharti yaliyokubaliwa wakati wa kusainiwa Novemba 8, mwaka jana.
Barua ya Kaseja iliyotumwa kupitia wakili wake, Mbamba & Co Advocates, Kaseja imesema wakati wa kusainiwa Mkataba huo ilikubaliwa malipo ya Sh. Milioni 40 yafanyike kwa awamu mbili.
Alisema awamu ya kwanza, alilipwa Sh. Milioni 20 baada ya kusaini Mkataba huo, na ikakubaliwa fungu lililobaki apatiwe Janauri 15, mwaka jana na kwa sababu malipo ya fedha ndio msingi wa Mkataba wenyewe, kushindwa kulipa fedha hizo kunaondoa uhalali wake.hivyo, Yanga SC baadaye ilikuja kusema imekwishamlipa fedha zake zote Kaseja na hana anachodai, ingawa kipa huyo alifungua madai mapya, akidai anachukiwa na kocha wa makipa, Juma Pondamali hivyo hana amani ya kufanya kazi.
Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu
Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:
NAFASI ZA AJIRA
JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA
GOODLUCK
Ni kwa kuwa alikuwa hatakiwi tena na simba ndio akajiunga na Yanga,Kaseja ni Simba damu,nilishangazwa sana kusikia Yanga wanamsajili.
ReplyDeleteNi kama Mrisho Ngasa anavyoipenda Yanga,