Kauli Mpya ya Mkapa Kuhusu Ukawa Baada ya ile ya Malofa na Wapumbavu Hii Hapa

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Rais mstaafu, Benjamin Mkapa ameponda kauli ya vyama vya upinzani kuwa vitaleta mabadiliko, akisema kazi hiyo tayari imefanywa na CCM.
Akizungumza kwenye Uwanja wa Uhuru mjini Bukoba wakati wa uzinduzi wa kampeini za wagombea wa chama hicho mkoani Kagera, Mkapa alisema chama pekee kilichobobea katika ukombozi ni CCM na Serikali zake zilizotangulia.
Kiongozi huyo wa Serikali ya Awamu ya Tatu alisema kuwa lengo la vyama vya upinzani ni kuing’oa CCM na lengo la chama hicho tawala ni kuendelea kushika dola, hivyo upinzani unatakiwa kujifunza hadi baada ya miaka 50.
Alitaja miradi mbalimbali ya maendeleo iliyotekelezwa kwa awamu tofauti kuwa ndiyo aina ya mabadiliko ya maendeleo wanayohitaji wananchi, akitaja uwanja wa ndege wa Bukoba na barabara za lami.
“Hayo ndiyo mabadiliko ya maisha ya Watanzania huwezi kuleta ajira kwa kutamka tu, tulianzisha wilaya na mikoa mipya ili kuchochea maendeleo ya wananchi na maisha yao hayo ndiyo mabadiliko,’’ alisema Mkapa.
Jana, alionekana kuzungumza kwa tahadhari kwa kile alichodai akiwaeleza wapinzani ukweli wanadai ana jeuri.
Hata hivyo, katika hotuba yake alishindwa kujizuia na kutamka neno mbumbumbu na kusema hataki kuwazungumzia.
Kabla ya kumkaribisha Mkapa kuhutubia, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kagera, Costancia Buhiye alisema wagombea wote wamepita kwenye mchujo sahihi na kutamba kwamba chama hicho kimejipanga kupata ushindi.
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Top Post Ad