Magufuli Aponda Ahadi Ya Lowassa Kufuta Umasikini Ndani Ya Siku 100......Asisitiza Kuwa Serikali Yake Haitawavumilia Watu Wavivu

 AJIRA ZA UHAKIKA NJE NJE, BONYEZA HAPA

Mgombea urais wa CCM, Dk John Magufuli amewataka wananchi kujipanga kufanya kazi kwa sababu Serikali yake haitavumilia watu wavivu.

Akihutubia mkutano wa kampeni katika Uwanja wa Shule ya Msingi Misungwi jana, Dk Magufuli alisema hata vitabu vya dini vimeelekeza kwamba asiyefanya kazi na asile, hivyo wanaoahidi vitu vya bure wanawadanganya Watanzania.

“Tujipange kufanya kazi, hata maandiko ya vitabu vitakatifu yanasema, asiyefanya kazi asile… Misungwi nitaibeba kwa nguvu zangu zote nikichaguliwa,” alisema.

Pia alisema nyumba za tembe ambazo zinaahidiwa na wagombea wenzake kwamba zitaondolewa ndani ya siku 100 ni uongo hivyo wasisikilizwe, bali atakachofanya ni kuhakikisha bei ya vifaa vya ujenzi inapungua na ameanza na saruji.

Alisema anatambua kuwa wilaya hiyo inakabiliwa na tatizo la maji na kuwaahidi wananchi kulishughulikia na wasimsumbue mbunge wao na kwamba anapoahidi kutoa Sh50 milioni kila kijiji nchini watu wanamshangaa lakini Serikali ina fedha, nyingine zilikuwa zinatafunwa na mafisadi.

“...Ndiyo maana baada ya kusikia nimetangazwa mengine yakakimbia… hivi sasa wanasema Serikali haijafanya chochote wakati wengine wamezeekea humu mpaka wakang’oka meno na kuwekewa ya bandia, mbona hawakuondoka muda wote?” alihoji Dk Magufuli.

Mgombea huyo huku akichomeka lugha ya Kisukuma kila mara, alisema ujenzi wa barabara ya Usagara – Kisema ukikamilika, malori yatakuwa hayaruhusiwi kuingia katikati ya mjini wa Mwanza. Aliahidi kufufua viwanda vya kuchambua pamba ili kuleta mabadiliko ya kweli.

Dk Magufuli aliahidi kufufua kilimo cha pamba kwa kuhakikisha mkulima anapata pembejeo na kunufaika na zao hilo na kwamba, haiwezekani pamba ilimwe Tanzania Ulaya wavae nguo mpya halafu Watanzania waletewe mitumba.

Hata hivyo, mgombea huyo akiendelea kutoa ahadi sauti za wanawake zilisikika zikimtaka kuzungumzia samaki kazi ambayo ndiyo wanayoitegemea kiuchumi, hivyo akalazimika kutamka kuwa atafuta ushuru unaoonekana kuwa kero.

“Nitafufua Chuo cha Kilimo Ukiriguru na kutumia wataalamu wake kuboresha kilimo cha pamba,” alisema.

Mgombea ubunge Jimbo la Misungwi, Charles Kitwanga alisema kuna sifa ya Dk Magufuli ambayo haijatajwa nayo ni ubunifu, kwani alianzisha mfuko wa kujenga barabara kwa fedha za ndani hali iliyowashangaza wafadhili.

“Hizi barabara tunazotaja kama siyo yeye zisingekuwapo, mnakumbuka wafadhili walikuwa wanakataa kutukopesha, akaanzisha mfuko wa kujenga barabara mpaka wafadhili wanauliza fedha zitakapopatikana, akawaambia tunazo,” alisema.

Kitwanga alimwomba mgombea huyo kuwajengea hospitali ya wilaya na kiwanda cha kusindika nyanya, zao linalolimwa kwa wingi.
Mpekuzi blog
----

Utamu wa audio book ya SIRI YA PADRE NA MKE WANGU hauna mfano, sikiliza Sehemu ya 1 bure, Sehemu ya 2 Tsh 2000 tu

Nusu ya mapato ni kwa ajili ya wagonjwa wasiojiweza, Lipia uburudike huku ukitoa sadaka Safi,ni www.makapedia.com au bofya kitabu hapo chini:



 

-------------------

NAFASI ZA AJIRA 

JIUNGE NA AJIRA YAKO TELEGRAM GROUP HAPA

INTERNSHIP VACANCIES

GOVERNMENT VACANCIES

NGO'S VACANCIES 

GOODLUCK

Top Post Ad